• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vijana washauriwa kujiajiri kupitia kazi za ubunifu wa mikono

Imewekwa tarehe: May 12th, 2021

SHUGHULI za ubunifu na ukuzaji wa talanta ni njia sahihi ya kujiajiri vijana na kuweza kujitegemea na kukuza uchumi wao na taifa na kuepuka na utegemezi.

Kauli hiyo ilitolewa na mbunifu Dorothea Msigwa wakati akielezea fursa za ubunifu kwa vijana katika banda la Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) katika maonesho ya kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu yanayoendelea katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma.

Msigwa alisema kuwa katika kipindi ambacho tatizo la ajira ni kubwa vijana wanatakiwa kufikiria njia mbadala ya kujiajiri. “Kwa vijana wote nawashauri tu talanta na ubunifu vinalipa. Umefika wakati kwa vijana kujituma katika kufanya kazi kwa sababu mwanzo wa kitu kimoja ndio njia ya mafanikio kwa kitu kingine, ndiyo imani yangu” alisema Msigwa.

Msigwa ambaye ni mwanafunzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini ni binti anayependa kazi za mikono. “Mimi nimebuni shughuli ninazofanya kwa mikono yangu. Ninatengeneza mapambo ya ukutani, ‘table mats’, maua ya urembo wa ndani na mazulia ya milangoni” alisema mbunifu huyo.

Alisema kuwa ubunifu wake unamsaidia kujiajiri mwenyewe na kuondoa tatizo la ajira. “Ubunifu wa kazi za mikono unanisaidia pia kuepukana na tamaa mbalimbali zinazotokana na masuala ya kiuchumi” alisema Msigwa.

Akiongelea soko la bidhaa zake, alisema kuwa soko lipo. “Soko ni kutokana na wewe mwenyewe muuzaji unavyo changamka kupata wateja. Kadri unavyojituma sana kutafuta wateja ndivyo soko linavyozidi kuwa kubwa. Jamii inayonizunguka inapendezwa sana na bidhaa zangu, si watoto, wakubwa hata wazee, kwa kifupi wao ndio wa kwanza kuniunga mkono” aliongeza Msigwa.

Mwanafunzi huyo mbunifu alikishukuru chou chake kwa msaada wa mawazo na maeneo ya kimkakati anaopata. “Chuo kimekuwa cha kwanza kutangaza bidhaa zangu kiujumla” alisema Msigwa.

Akiongelea jinsi ya kuweka mizania ya muda wa masomo na shughuli za ubunifu wa kazi za mikono anazofanya, alisema kuwa anajitahidi kuweka mizania sawa. “Kiukweli kila kitu na muda wake. Najitahidi sana kubana muda wa masomo na muda wa kufanya kazi zangu za ubunifu. Hivyo, muda wangu unakuwa umepangwakikamilifu.

Mwanafunzi huyo mbunifu alisema kuwa alipata mtaji wa kuanzisha shughuli zake za ubunifu kutokana na fedha za matumizi ya shule alizokuwa akipewa na mzazi. “Kwa mtaji wa kuanzia, kama nilivyo kueleza awali, napenda kazi za mikono hivyo, kwa kuwa mimi nasoma, mzazi alipokuwa akinitumia fedha ya matumizi nabakiza kama ya akiba na ndio mtaji wangu ukawa hivyo” alieleza kwa kujiamini.

Ikumbukwe kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inaendesha Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) kwa madhumuni ya kutambua, kuadhimisha, kujenga, kukuza na kuendeleza ubunifu wa watanzania katika nyanja za sayansi na teknolojia ili kuchangia juhudi za kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa kati unaoendeshwa na viwanja.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.