• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vikundi 109 kukopeshwa Milioni 853 Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: December 17th, 2019

WAJASIRIAMALI  jijini Dodoma wametakiwa kutumia fursa ya mikopo wanayoipata katika kuendeleza miradi yao ipasavyo sambamba na shughuli wanazotumia katika kuomba fedha hizo.

Wito huo umetolewa leo na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Sharifa Nabalang'anya katika mafunzo ya siku tatu kwa wajasiriamali juu ya  matumizi sahihi ya mikopo yanayoendelea katika ukumbi wa shule ya Sekondari Umonga jijini hapa.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa elimu inayotolewa kwa wajasiriamali jijini hapa ikiwa ni hatua mojawapo ya kuwajengea uwezo katika kukabiliana na changamoto kubwa wanayokumbana nayo juu ya matumizi sahihi ya mikopo hiyo.

"Tunatoa mafunzo kwa vikundi 109 vya wajasiriamali wa makundi matatu ambayo ni vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kama sheria ilivyopitishwa na kuagiza Halmashauri zote Tanzania kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo kwa makundi haya.

"Tunatarajia kutoa shilingi milioni 853 kwa vikundi  hivi, hivyo kabla hatujatoa fedha ni utaratibu wetu kuwapa mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, usimamizi wa miradi na namna ya kurejesha mikopo hii," alisema Nabalang'anya.

Pia amewasisitiza wajasiriamali jijini hapa kuhakikisha mafunzo wanayoyapata wanayatumia vyema ili waweze kujikwamua kiuchumi kuanzia ngazi ya familia na hata taifa kwa ujumla.

"Ujasiriamali unalipa na sasa hivi Dodoma ni jiji, tumieni fursa hii hakikisheni mnaongeza bidii katika shughuli mnazozifanya, pia hakikisheni mnajitangaza kupitia bidhaa mnazozalisha mkizingatia katika ubora wa kile mnachozalisha", alisema Afisa huyo.

Christopher Magesa ni moja kati ya wajasiriamali aliyepata mafunzo hayo, huku akisisitiza kuwa ataakuwa balozi mzuri kwa wengine katika kufikisha elimu hii kwa wajasiriamali ambao hawajapata mafunzo hayo.

"Nimejifunza mengi katika mafunzo hayo, yamenijengea uwezo wa kujiamini, nimepata pia kujua kwa kina kuhusiana na masuala ya mikopo na  jinsi ya kuirejesha, kubwa zaidi nimefurahi kuwa na mikopo hii kutolewa bila riba ya aina yoyote," alisema Magesa.

Mafunzo hayo yamewakutananisha wajasiriamali jijini hapa na wataalam wa vitengo mbalimbali  wakiwemo wataalam kutoka idara ya Mipango na Fedha, Mifugo, Kilimo na Ushirika katika kufanikisha wajasiriamali kufanya vitu walivyokusudia  katika miradi yao kwa ufanisi zaidi.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Sharifa Nabalang'anya akiongea wakati wa mafunzo kwa wajasirimali wanaotarajiwa kukopeshwa mikopo isiyo na riba kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


Wana vikundi wakisikiliza kwa makini maelekezo kuhusiana na matumizi bora na endelevu ya mikopo wakatayopewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.