• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vikundi vyatakiwa kujipanga na kuwajibika kufanya usafi

Imewekwa tarehe: June 4th, 2023

Na. Dennis Gondwe, IPAGALA

Vikundi na makampuni yaliyopewa dhamana ya kufanya usafi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma yametakiwa kujipanga na kuwajibika kufanya usafi katika maeneo yao kwa mujibu wa mikataba yao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri katika maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani leo tarehe 4 Juni, 2023 baada ya kushiriki zoezi la usafi wa Mazingira wa pamoja na wananchi wa Kata ya Ipagala jijini Dodoma.

Shekimweri alisema kuwa makampuni na vikundi vilivyopewa kazi ya kufanya usafi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma viwajibike kikamilifu kutekeleza majukumu yao. “Si vema tunafanya mazoezi ya usafi kama haya wakati kuna vikundi na makampuni ambayo tunayalipa kwa ajili ya kufanya usafi ila hayafanyi usafi huo kwa mujibu wa mkataba. Nataka kuona thamani ya fedha ikionekana. Halmashauri ya Jiji simamieni makampuni haya na vikundi hivi. Wakati mwingine muwakate mapato yao ili watekeleze majukumu yao vizuri. Natamani kuona magari ya usafi ni magari mazima. Siyo gari lenyewe na kuchukulia uchafu lenyewe linatembea na kuacha uchafu nyuma yake au kutoa harufu mbaya” alisema Shekimweri.

Aidha, aliwataka wakazi wa wilaya ya Dodoma kufanya suala la usafi kuwa tabia. “Usafi wa Mazingira iwe ni tabia yenu isiwe ni usafi kwa matukio kama haya ili kupiga picha za mitandao. Usafi ukiwa ni tabia yetu, mtu hatahitaji kuelekezwa, ataona ni wajibu kuishi katika Mazingira safi na salama. Nitoe rai kwa wafanyabiashara kufanya usafi katika maeneo yetu. Zaidi tuwe na vifaa vya kuhifadhia uchafu” alisema Shekimweri.

Aliwataka maafisa watendaji wa kata na mitaa kushirikiana na maafisa afya kukagua maeneo ili kubaini hali ya usafi. “Kwangu jambo hili ni changamoto lakini pia ni fursa, kuna sheria ndogo zitumieni kuongeza mapato. Mkikuta mazingira ni machafu pigeni faini” alisema.

Kwa upande wa Mkuu wa Kitengo cha usimamizi wa Usafi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa halmashauri itaedelea kuhimiza wananchi kushiriki kufanya usafi wa Mazingira. “Jukumu letu ni kuhakikisha makao makuu ya nchi yanakuwa safi” alisema Kimaro.

Maadhimisho ya siku ya Mazingira yatafikia kilele chake tarehe 5 Juni, 2023, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika viunga vya Soko la wazi la Machinga jijini Dodoma chini ya kaulimbiu “Pinga uchafuzi wa Mazingira unaotokana na taka za plastiki”





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.