• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Afya waagizwa kukagua Vifaa vyakunawia mikono Vilabuni

Imewekwa tarehe: October 15th, 2022

Na. Sifa Stanley, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri amewaagiza Maafisa Afya wa Jiji la Dodoma kufanya ukaguzi katika Vilabu vya pombe ili kuhakikisha kuwa maeneo hayo kuna vifaa vya kunawa mikono na matundu yakutosha ya Vyoo.

Alitoa maagizo  hayo katika maadhimisho ya siku ya unawaji mikono duniani ambayo kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yalifanyika katika shule ya msingi Mtumba Kata ya Mtumba.

Akielezea faida za kunawa mikono kwa afya ya binadamu, Mkuu huyo alisema kunawa mikono kutaisaidia jamii kuepukana na magonjwa ya mlipuko na kuifanya jamii kuwa imara na yenye afya.

Ili kuhakikisha Wilaya ya Dodoma inajilinda na kujikinga na magonjwa ya mlipuko, Mkuu wa Wilaya aliagiza Maafisa Afya wa jiji la Dodoma kupita katika maeneo ya Vilabu vya pombe ili kukagua kama maeneo hayo wameweka vifaa vya kunawa mikono, na ikiwa hakuna vifaa vya kunawa mikono basi kilabu kifungwe mkapa watakapoweka vifaa hivyo.

“Nasisitiza kunawa mikono ukiingia msalani na nasisitiza kunawa mikono baada ya kutoka na kabla ya kujichanganya na jamii nyingine, lakini imekuwa ni kawaida sana ukitembea kwenye vichochoro na kwenye vilabu vya pombe unakuta mtu anaingi kichakani anajisaidia na humuoni akinawa mikono wala kujisafishisha kwa kutumia kitakasa mikono na narudi anajichanganya na jamii nyingine,

Sasa nielekeze ya kwamba  hata katika vilabu vya pombe Maafisa Afya wa jiji letu wapite wahakikishe kuwa maeneo hayo kuna sehemu kwaajili ya kunawa mikono na ili wamiliki waendelee kufanya biashara ni lazima waweke maeneo ya kunawa mikono na matundu yakutosha ya vyoo, kwa kufanya hivyo nina imani tutapambana na magonjwa ya mlipuko”, alisisitiza Shekimweri.

Naye Msafiri Njani mkazi wa Kata ya Mtumba, aliuomba uongozi wa Kata ya Mtumba kuendelea kutoa elimu juu ya unawaji mikono ili kuinusuru jamii ya Mtumba dhidi ya magonjwa, lakini pia aliahidi kutoa hamasa ya unawaji mikono kwa vijana wenzake na wananchi wote kwa ujumla ili kuepuka magonjwa ya mlipuko.

“Mimi nitafata sheria na kanuni zote za unawaji mikono na nitaendelea kuwaelimisha vijana wenzangu kunawa mikono. Ungozi wa kata nawaomba wazidi kuhamasisha watu kunawa mikono kwasababu saivi kuna magonjwa mengi ya mlipuko ambayo ni hatari sana”, alisema Njani.

Naye Evelina Kusenha, mwanafunzi wa shule ya msingi Mtumba alielezea faida za kunawa mikono na kuwasisitiza wanafunzi wenzake kuendeleza desturi ya kunawa mikono wawapo shuleni na hata nyumbani ili kujilinda dhidi ya magonjwa.

“Kuna faida nyingi na umuhimu mkubwa wa kunawa mikono, kwasababu inasaidia kuepuka magonjwa kama vile kuhara na kuhara damu, pia kunawa mikono kunasaidia kuepuka magonjwa ya mfumo wa upumuaji, wanafunzi wenzangu tuendelee kunawa mikono kwa maji safi na sabuni”, alieleza Kusenha.

Ifikapo Oktoba 15 ya kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya unawaji mikono Duniani, lengo likiwa ni kuendelea kujenga ulimwengu wenye afya na kusaidia kupigana vita dhidi ya magonjwa mbalimbali ya mlipuko.Katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma maadhimisho haya yalifanyika katika Shule ya Msingi Mtumba iliyopo Kata ya Mtumba yakiwa yamebeba kaulimbiu isemayo “Tuungane pamoja kuhakikisha usafi wa mikono kwa wote”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.