• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Viongozi wa Dini Dodoma watoa neno kabla ya Uchaguzi wa Oktoba 28

Imewekwa tarehe: October 24th, 2020

KATIKA kusisitiza amani na utulivu wakati wa kumalizia kampeni na kisha kupiga kura Oktoba 28, mwaka huu, viongozi wa dini wamewataka wananchi kujitokeza kupiga kura na mara wakipiga kura waende nyumbani kupumzika wasizagae mitaani.

Viongozi hao waliongea kwa nyakati tofauti katika mkutano wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dodoma jijini hapa jana wakinukuu vitabu vitakatifu vya Biblia na Korani, walisema kupiga kura ili kuchagua viongozi si haramu, hivyo kila kiongozi wa dini katika madhabahu na mimbari yake anatakiwa kwenda kuhamasisha waamini na waumini wake wenye sifa kwenda kupiga kura kwani hilo ni takwa la kikatiba na kidini pia.

Akiufungua Mkutano wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge aliwataka viongozi hao kutumia nafasi zao kuhubiri amani na utulivu na asiwepo mtu atakayetumia uchaguzi kuwa kigezo cha kuwagawa wananchi na ushindani usiweke rehani amani iliyodumu miaka mingi hapa nchini.

Mchungaji Kanisa la Calvary Assemblies of God Kisasa Relini jijini hapa, Visenti Malenda alisema ili kudumisha amani na utulivu baada ya kupiga kura Oktoba 28, 2020 wananchi wote wanatakiwa kuambiwa kuondoka vituoni na kwenda kupumzika nyumbani.

Mchungaji Malenda aliongeza kuwa inatakiwa kutolewe msisitizo wa kutoruhusu vijana kurandaranda na kuendeleza hoya hoya mitaani kunachangia kuwaingiza katika matatizo ambayo si ya lazima na hawastahili.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini mkoani Dodoma, Sheikh Mustaferpha Shaban alisema viongozi wa dini hivi karibuni wengine wamepotoka kwa kunadi sera, kutangaza wagombea na kushabikia vyama vya siasa kazi ambayo si wajibu wao.

Aliwataka viongozi wa dini kuacha kujiingiza katika masuala ya siasa na kuwaachia wanasiasa, wao kama viongozi wa dini wanatakiwa kuonya na kuonesha mema, “Kuingia katika jukwaa la kampeni na kunadi vyama, wagombea au kunadi sera za vyama si jukumu la viongozi wa dini,”

Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Philadelpia Assembly of God, Dkt. Yohana Masinga alisema Taifa la Tanzania limempa nafasi Mungu na kiongozi wake akaamua kumpa Mungu nafasi wakati wa Corona, vile vile viongozi wa dini wanatakiwa kuomba ili Mungu uchaguzi upite salama.

Vilevile, Mjumbe wa Baraza la Masheikh Mkoa wa Dodoma Sheikh Kisusu Mvumbo alisema, amani inatakiwa kutamalaki nchini kwa kuhakikisha kwamba wao kama viongozi wa dini wanaombea  uchaguzi unakuwa wa amani na utulivu.

Akichangia Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Dkt. Brown Mwakipesile alisema, Taifa la Tanzania linamhitaji Mungu wakati wa uchaguzi ili kupata viongozi watakaolivusha kwani kwa kumtegemea yeye kila jambo litawezekana na uchaguzi utakuwa wa amani.

Katibu wa Vijana katika Kanisa la Anglican mkoani Dodoma, Mchungaji Cosmasy Maginda alisema katika kuepusha malalamiko kila chama hata kama kidogo kinatakiwa kupewa haki mfano kila chama kinastahili kupata ulinzi wa kutosha hata kama kina wafuasi wachache hawana budi watendewe haki ya kupewa ulinzi.

Ndipo Askofu wa Kanisa la Mlima wa Moto mkoani Dodoma, Sylvanus Komba aliomba uongozi wa Vyama vya Siasa kuendelea kutoa elimu kwa viongozi mbalimbali wakiwamo wa dini wakati wote badala ya kungoja wakati wa uchaguzi tu, kwani ng’ombe hanenepi siku ya mnada.

Baadae, Afisa Tawala Mwandamizi wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Prudensia Kwabila akasema, vyama vya siasa vizingatie sheria za nchi zikiwemo za uchaguzi na sheria ya gharama za uchaguzi, sheria za vyama vya saisa na kanuni zake ili kudumisha uhusiano mwema, utii wa sheria bila shuruti na uvumilivu wa kisiasa pamoja na amani na utulivu.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Josephat Maganga aliwataka viongozi wa dini kushikamana na viongozi wa serikali kuhakikisha katika mkoa wa Dodoma uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu ili kupata viongozi watakaoleta maendeleo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy alisema, viongozi wa kanisa wakiwemo maaskofu, masheikh, wachungaji, maimamu na viongozi wengine wana nafasi ya kuivusha nchi kwa kuomba uchaguzi uwe wa amani, upendo na mshikamano.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (wa pili kulia), Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoani Dodoma Sheik Mustaferpha Shabani (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Josephat Maganga (kushoto) na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Maduka Kessy (wa pili kushoto) wakiwa katika meza kuu wakati wa kikao Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dodoma.

Baadhi ya viongozi wa Dini wakisilikila wakati kikao kikiendelea.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.