• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Viongozi wa vyama vya siasa Jiji la Dodoma watakiwa kufanya siasa za kistaarabu

Imewekwa tarehe: November 22nd, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

VIONGOZI wa vyama vya siasa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ili Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kufanyika kwa amani na utulivu.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na wadau wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ofisini kwake leo wakati akiwaelezea mwenendo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Dkt. Sagamiko alisema kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa Kalenda ya Uchaguzi zinafanyika siku saba kabla ya tarehe ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Hivyo, kampeni zilianza jana tarehe 20 Novemba, 2024 baada ya vyama vya siasa kuwasilisha ratiba ya mikutano ya kampeni kwa Msimamizi wa Uchaguzi. Ratiba hizo zilishawasilishwa kwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Dodoma. Mkuu wa Polisi Wilaya anawajibu wa kuhakikisha ulinzi na usalama katika mikutano ya kampeni. Mikutano ya kampeni itaanza saa mbili asubuhi na itamalizika saa kumi na mbili kamili jioni ya kila siku ya kampeni”.

Akiongelea mabadiliko ya ratiba kwa vyama vya siasa pale inapobidi alisema kuwa yawasilishwe kwa maandishi. “Iwapo chama cha siasa chenye mgombea kitahitaji kufanya mabadiliko ya ratiba ya mikutano ya kampeni kitatakiwa kuwasilisha kwa maandishi mapendekezo ya mabadiliko hayo kwa Msimamizi wa Uchaguzi na mapendekezo hayo kuridhiwa kwa mujibu wa kanuni. Baada ya mapendekezo hayo kuridhiwa na vyama vya siasa yatawasilishwa kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya kwa ajili ya kupatiwa ulinzi kwenye mikutano ya kampeni” alisema Dkt. Sagamiko.


Msimamizi huyo wa uchaguzi alisema kuwa yapo masharti ya kampeni za uchaguzi ambayo wagombea na vyama vya siasa hawaruhusiwi kufanya katika mchakato wa uchaguzi. Masharti hayo yanalenga kuhakikisha kampeni zinafanyika kistaarabu na kudumisha amani na utulivu. “Kutoa maneno yanayolenga uvunjifu wa amani au kuchochea vurugu. Kutumia rushwa wakati wa uchaguzi, kutoa maneno ya kashfa na matusi na kutumia ubaguzi wa jinsia, dini na kabila” alisema Dkt. Sagamiko.


Aidha, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kufuatilia na kusikiliza kampeni za vyama vya siasa ili kufahamu sera za wagombea mbalimbali. Kampeni za vyama vya siasa zitawasaidia kufanya maamuzi siku ya kupiga kura tarehe 27 Novemba, 2024, aliongeza.


MWISHO




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.