• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Viwandani Sekondari pandisheni taaluma – Prof. Mwamfupe

Imewekwa tarehe: July 16th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SHULE ya sekondari Viwandani iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetakiwa kupandisha kiwango cha taaluma ili kiendane na hadhi ya kuwepo makao makuu ya nchi kwa kuwatengenezea wanafunzi mazingira bora ya kujifunzia na walimu mazingira bora ya kufundishia.

Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alipoingoza kamati hiyo kutembelea na kukagua hali ya ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa uzio wa shule ya sekondari Viwandani jijini hapa.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa kiwango cha taaluma hakiridhishi na kusadifu uwepo wa shule hiyo makao makuu ya nchi. “Shule hii ipo hapa usoni kabisa mwa Jiji, lazima mjitahidi kupandisha hali ya taaluma. Hatuwezi ongelea elimu bora wakati wanafunzi hawapo madarasani. Ndiyo maana tumejenga madarasa hapa ili wanafunzi wapate sehemu ya kusomea na kujadili ubora wa elimu tunayowapa. Mwalimu lazima uwe na takwimu zote muhimu za shule katika viganja vya mikono yako” alisema Prof. Mwamfupe.

Prof. Mwamfupe ambaye ni Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma aliushauri uongozi wa shule hiyo kupanda miti ya aina mbalimbali. “Umefika wakati wa shule kupanda miti ya kutosha shuleni hapa. Wekeni vimbwete ili wanafunzi wapate sehemu nzuri ya kujisomea nje ya madarasa. Vimbwete na kivuli cha miti vitasaidia kuboresha mazingira ya wanafunzi kujisomea na kupandisha ufaulu” alisema Prof. Mwamfupe.

Katika hatua nyingine, Meya huyo aliwashauri walimu wa shule hiyo kuanzisha umoja utakaokuwa kimbilio lao wakati mgumu. “Niwashauri kuanzisha umoja wenu hapa ili uweze kuwasitiri walimu mnapokumbana na changamoto, inaweza kuwa Saccos ya walimu” alisema Prof. Mwamfupe.

Akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Shule ya Sekondari Viwandani, Mchumi katika halmashauri hiyo, Abeid Msangi alisema kuwa Halmashauri ilipeleka shilingi 20,000,000 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa uzio shuleni hapo.

Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilifanya ziara ya kikazi kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi iliyotekelezwa na jiji hilo kwa kipindi cha robo ya nne (Aprili-Juni, 2022).

Mhe. Sospeter (kushoto) akimsikiliza mwakilishi wa Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Fredrick Mwakisambwe akitoa maelezo hali ya taaluma shuleni Viwandani.

Matangazo

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA MAKARANI WAOGOZAJI WAPIGA KURA October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.