• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vyama vya Siasa vyashauriwa kufanya kampeni za kistaarabu

Imewekwa tarehe: September 23rd, 2019

VYAMA vya siasa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma vimetakiwa kufanya kampeni za kistaarabu wiki moja kabla ya siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa ngazi ya Mtaa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa za mwaka 2019.

Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi huo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro (pichani kushoto) alipokuwa akitoa maelezo kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa ngazi ya Mitaa utakaofanyika tarehe 24 Novemba, 2019, kwa viongozi wa vyama vya siasa na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya Kata katika Halmashauri hiyo kwenye kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji leo.

Kimaro alisema kuwa kampeni za uchaguzi zitafanyika wiki moja kabla ya siku ya uchaguzi. “Kampeni zitafanyika kwa muda wa siku saba yaani kuanzia tarehe 17/11/2019 hadi 23/11/2019 saa 2:00 asubuhi na kumalizika saa 12:00 jioni kila siku” alisema Kimaro. Alivitaka vyama vyote kufanya kampeni za kistaarabu muda utakapofika kwa mujibu wa kanuni kwa kuzingatia maslahi mapana ya amani ya nchi.

Kuhusu uandikishaji, alisema kuwa uandikisha utafanyika kuanzia tarehe 8/10/2019 hadi 14/10/2019 kwenye vituo vya kupigia kura vilivyopo katika mitaa iliyopo kwenye orodha iliyotangazwa na serikali ya maeneo ya utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Upigaji kula utafanyika kwenye vituo vya kupigia kura vilivyopo kwenye mitaa iliyoko kwenye orodha ya maeneo ya utawala ya Halmashauri ya Jiji” aliongeza Kimaro. Vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni, aliongeza.

Msimamizi huyo wa uchaguzi alizitaja sifa za mtu anayestahili kuandikishwa kuwa awe ni raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au zaidi. Sifa nyingine alizitaja kuwa ni mkazi wa eneo la mtaa husika na awe amejiandikisha kupiga kura katika Mtaa husika. Sifa nyingine mtu huyo hana ugonjwa wa akili uliothibitishwa na daktari anayetambulika na serikali au bodi ya utabibu.

 Awali akimkaribisha msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Uchaguzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hidaya Maeda alisema kuwa kanuni za uchanguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa ngazi ya vijiji, vitongoji na mitaa za mwaka 2019 zinaelekeza msimamizi wa uchaguzi kutoa maelezo kuhusu uchaguzi wa serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 24 Novemba, 2019.

Maeda alisema kuwa lengo la maelezo hayo ni kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa amani pasipokuwa na changamoto zozote. Akiongelea ushiriki wa maafisa watendaji wa Kata katika uchaguzi huo, aliwataja kuwa ni wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi huo ngazi ya Kata kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa za mwaka 2019.

Kikao hicho kilihudhuriwa na vyama vya siasa vya CCM, Chadema, ACT Wazalendo, UMD, Sauti ya Umma, NCCR Mageuzi, CUF na Demokrasia makini.


Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Msimamizi wa Uchaguzi wa Jiji la Dodoma na wawakilishi wa Vyama vya siasa kutoka Jiji la Dodoma kwenye kikao kilichofanyika tarehe 23 Septemba, 2019 katika Ukumbi mkubwa wa Mikutano wa Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.