• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vyuo Vikuu vyote kufunguliwa Juni 1, 2020 - Rais Magufuli

Imewekwa tarehe: May 21st, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza kuwa vyuo vikuu vyote nchini vitafunguliwa kuanzia Juni 1, 2020.

Wanafunzi wa kidato cha sita nchini nao ambao wanakaribia kufanya mitihani ya kumaliza elimu ya sekondari pia watarejea shuleni siku hiyo.

Rais Magufuli amesema kuwa wameamua kufanya hivyo kwa kuwa kasi ya ugonjwa wa Covid19 imepungua Tanzania.

"Hali ya ugonjwa wa Corona nchini imeshuka sana hivyo, sisi kama serikali tumeamua kufungua vyuo vyote Juni 1, 2020 kwahiyo Wizara zinazohusika zijiandae ili vyuo vitakapofunguliwa isitokee kero zingine," ameeleza Magufuli.

Magufuli hata hivyo amesema kwa wanafunzi wengine bado kunahitajika muda wa kufanya tathmini.

"Kwa shule za msingi na madarasa mengine ya sekondari tujipe muda kidogo...tutatathmini maendeleo ya wengine waliofungua kwanza. Hawa wa chuo kikuu ni watu wazima, wanajitambua," amesisitiza rais Magufuli.

Taasisi zote za elimu nchini Tanzania zilifungwa katikati ya mwezi Machi mara baada ya Tanzania kuthibitisha mgonjwa wa kwanza wa virusi vya Corona nchini.

Rais Magufuli pia ameatangaza kuwa tarehe hiyo ya Juni 1 ndiyo michezo yote ikiwemo Ligi Kuu ya Kandanda itarejea.

Michezo ni muhimu hivyo tumeamua pia kufungua michezo kuanzia Juni 1, 2020, taratibu za kuangalia na kushangilia mpira zitapangwa vizuri na Wizara ya Afya pamoja na Wizara ya Michezo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema kupitia mtandao wa Twitter kuwa baada ya kauli hiyo ya rais sasa ni rasmi kwa timu zote kuanza mazoezi.

Mapema wiki hii Rais wa Shirikisho la Kandanda nchini Tanzania (TFF) Wallace Karia akiongiea na BBC alisema kuwa wanaendelea na maandalizi ya ndani wakisubiri mwongozo rasmi wa serikali.

Karia alisisitiza kuwa michezo ya ligi itakaporejea, mashabiki hawataruhusiwa uwanjani.

Aidha, Rais Magufuli pia amesema kati ya Mei 27 na 28 ndege za watalii zitaanza kuingia hapa nchini.

Hayo ameyasema asubuhi ya leo katika Ikulu ya Chamwino Dodoma kwenye hafla ya kuwaapisha viongozi kadhaa aliowateua hivi karibuni akiwemo Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel pamoja na mabalozi kadhaa.

Rais Magufuli alitangaza Jumapili iliyopita na kusisitiza hii leo kuwa kasi ya corona imepungua Tanzania.

"Kwa taarifa za leo wagonjwa wamepungua, Amana ilikuwa ina watu 198 leo wamebaki 12 tu, Mloganzila ilikuwa inalaza watu 30 leo wamebaki 6, Hospitali ya Kibaha kulikuwa na wagonjwa 50 leo wamebaki watu 22," rais Magufuli alisema siku ya Jumapili.

Mpaka sasa, watu 509 wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya corona nchini Tanzania, huku 183 wakipona na watu 21 kufariki dunia.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.