• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wadau wa Maendeleo wekezeni kwa Mwanamke wa Kijijini

Imewekwa tarehe: October 19th, 2022

WADAU wa maendeleo hasa wanaoshughulikia masuala ya wanawake wameaswa kuelekeza rasilimali na afua zaidi katika kuwasaidia wanawake wanaoishi vijijini ambao ndio wazalishaji wakubwa wa malighafi za viwanda na mazao ya chakula katika Kaya na ndio wachangiaji wakuu wa pato la Taifa.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameyasema hayo alipozungumza na wananchi katika kata ya Mang'ula, Halmashauri ya mji wa Ifakara, wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro aliposhiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mwanamke anayeishi kijijini, Oktoba 15, 2022.

Waziri Dkt. Gwajima amesema kuwa Wanawake hasa wa vijijini ndio wanapata changamoto nyingi zaidi kutokana na mgawanyo wa majukumu katika familia, uwezo mdogo wa kipato, elimu na ujuzi duni, mila na desturi kandamizi, ukubwa wa wategemezi katika Kaya na udhaifu wa miundombinu iliyopo Vijijini, hivyo ni muhimu sana kuimarisha ustawi na maendeleo yao ili kupunguza changamoto zinazowakabili.

"Serikali imeamua kuimarisha Ustawi na Maendeleo ya Mwanamke anayeishi kijijini ili kuleta mabadiliko endelevu yatakayonufaisha jamii kwa ujumla na kumpunguzia huyu mama anayeishi kijijini athari mbalimbali zinazotokana na mabadiliko ya Tabianchi ikiwa ni pamoja na Njaa, Ukame na Mafuriko yanayoweza kuleta madhara ya kuharibu Nyumba zilizo dhaifu". Amesema Mhe. Dkt. Gwajima.

Ameongeza kwamba Maadhimisho hayo yanatumika kuhamasisha Wadau kuelekeza Rasilimali kwa wanawake waishio vijijini ambapo matokeo yake ni yatawezesha kuainisha mbinu za kuamsha Ari ya Wadau kuboresha hali na mazingira ya vijijini kwa kutoa kipaumbele katika kushughulikia changamoto, mahitaji yao na kuunga mkono jitihada za Wanawake Waishio Vijijini na kuandaa Mifumo ya kukusanya Takwimu za mchango wa Wanawake Waishio Vijijini katika kuinua uchumi wa Taifa.

Aidha, Waziri Dkt Gwajima amesema majukumu hayo yatajenga uwezo wa Wanawake Waishio Vijijini kuthubutu kushiriki katika Siasa, Uongozi na nafasi za kutoa Maamuzi ili waweke msukumo katika kuelekeza Rasilimali, Nyenzo za Uzalishaji Mali na huduma za kifedha kwa Vikundi vya Wanawake na SACCOS zilizopo vijijini na kuelimisha jamii kuhusu Mila na Desturi kandamizi ili kuleta mgawanyo sahihi wa majukumu na Rasilimali katika familia na kupunguza mzigo wa kazi za Malezi, huduma kwa wanafamilia na kushiriki katika Uzalishaji mali kwa wanawake waishio vijijini.

Waziri Dkt. Gwajima amebainisha pia jitihada zinazofanywa Serikali katika kuwainua wanawake wanaoishi vijijini ni pamoja na kuwezesha marekebisho ya sheria ya mamlaka za Serikali za Mitaa inayotoa fursa kwa wanawake kupata asilimia 4 ya mkopo ya mapato ya ndani ya Halmashauri bil 28.1 ilitolewa kwa bikuni 4894 hadi mwaa 2021.

"Mkutano wa sita wa Baraza la uwezeshaji wannchi kiuchumi Taarifa zinasema kuwa kuna fursa zamikopo naprogramu 85 za uwezeshaji wananchi kiuchumi, kati ya hizo 75 ni za Serikali na 10 za binafsi ambapo kati ya hizo 24 ni za kumuwezesha mwananchi mmoja mmoja." alisema Waziri Dkt Gwajima

Mmoja wa Mkulima mwanamke Clara Male Mkulima amewashukuru wadau wanaoendelea kuwawezesha wanawake wa vijijini hasa wakulima na kutoa ushuhuda wake hadi sasa amefanikiwa kuunganishwa na masoko mbalimbali na kuweza kuuza mbegu za asili kwa wingi kupitia shirika la Pelum.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Sebastian Kitiku amesema Wizara inashirikiana na Wisara za Kisekta na Wadau wa maendeleo katika katika kuhakikisha wanawake hasa wanaoishi vijijini katika kuongeza nguvu za kuwawezesha Wanawake hao kujikwamua kiuchumi katika shughuli zao hasa Kilimo.

Naye Mwakilishi wa Chama Cha Mawakili Wanawake Tanzania (TAWLA) Sailasi Nyumba amesema kuwa lengo kuu la kuanzisha chama chao ni kutoa huduma za kisheria kwa wanawake hasa wanoishi vijijini ili waweze kusaidia kupunguza changamoto wanazokabiliana nazo katika shughuli zao za kiuchumi.

Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Anayeishi Kijijini yanaadhimishwa kwa mara ya tano nchini Tanzania, ambapo Lengo la maadhimisho haya ni kutambua mchango wa Mwanamke Anayeishi Kijijini katika Kilimo, uhakika wa chakula na kuinua uchumi wa Kaya na Taifa kwa ujumla.

Kaulimbiu ya maadhimisho haya kwa mwaka huu ni, "Mwanamke Aishiye Kijijini ni Mzalishaji Mkuu wa Chakula Tumuwezeshe".

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.