• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TRCA yakutana na wadau kuhimiza matumizi ya huduma za mtandao

Imewekwa tarehe: February 3rd, 2022

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kanda ya kati imefanya mafunzo kuhamasisha matumizi ya huduma za mtandao (broadband) kwa wadau wa huduma za mtandao, mafunzo haya yamefanyika leo katika ukumbi wa TCRA jijini Dodoma.

Akitoa salamu kwenye mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mkuu wa Kanda ya Kati Boniface Shoo amesema kuwa lengo la semina hiyo ni kuongeza matumizi na upatikanaji wa huduma bora za mtandao kwa wananchi, taasisi za serikali na watu binafsi.

Mafunzo hayo yametolewa kwa maafisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Mji Kondoa na Halmashauri za Wilaya ya Mpwapwa, Kongwa, Chamwino, Bahi, Chemba, na Kondoa. Aidha, kulikuwa na ushiriki wa watoa huduma za mtandao kutoka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Vodacom, Tigo, Airtel na Halotel.

Akiwasilisha mada katika mkutano huo, Afisa kutoka TCRA Anania Mashenene amezitaja faida za matumizi na huduma za mtandao kuwa ni pamoja na kurahisisha na kutanua wigo wa biashara, kupunguza muda na gharama, kukuza ubunifu na uvumbuzi, urahisi katika upashanaji habari na kufika maeneo mengi kwa wakati, kupunguza mianya ya rushwa na kurahisisha utoaji huduma mbalimbali na uendeshaji wa shughuli serikalini.

Huduma za mtandao zinatumika katika mifumo ya taasisi za serikali na binafsi, huduma za kijamii kama vile shule, hospitali, mifumo ya biashara, mitandao ya kijamii, mifumo ya malipo ya ankara na mifumo ya ulinzi kama vile kamera za usalama (CCTV) amesema Mashenene.

Akizungumzia wajibu wa Serikali na hasa Halmashauri katika kukuza matumizi ya mtandao na utoaji wa huduma bora, Mashenene amesema halmashauri zina wajibu wa kuainisha maeneo yenye uhitaji wa mtandao, kutenga bajeti mahsusi kwa ajili ya TEHAMA, kutengeneza mifumo itakayosaidia katika kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo elimu na afya.

Nao watoa huduma kwa upande wao walielezea huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi zao ikiwemo huduma za sauti na data kama vile mawasiliano ya simu, vituo vya kuhifadhia data (data center), huduma za simu bure (CUG), kutuma ujumbe mfupi kwa watu wengi (bulk sms), na matumizi ya mkongo wa taifa katika kutoa huduma hizo.

Washiriki walibainisha changamoto za upatikanaji wa mawasiliano katika baadhi ya maeneo ya Halmashauri zao na kupendekeza namna bora zitakazowezesha upatikanaji wa huduma bora kwa kutumia mtandao katika halmashauri zao.

Vile vile, Mashenene amesema kuwa TCRA itaendelea kuwahimiza watoa huduma kufikisha huduma za kimtandao kwenye maeneo ambayo huduma haipatikani au kuna upatikanaji hafifu.

Aidha, Serikali kupitia taasisi zake za TCRA na USCAF zitahakikisha uainishaji na ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya huduma za kimtandao katika maeneo yasiyo na mvuto wa kibiashara yanapewa kipaumbele ili kupata huduma hizo pia.

Washiriki wa semina pamoja na wawezeshaji kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na wawakilishi wa watoa huduma wakiwa katika picha ya pamoja (picha ya juu na chini).


Mwakilishi kutoka Airtel Bi. Delphina Msuya akielezea huduma zitolewazo na kampuni ya Airtel wakati wa mafunzo kwa wadau wa huduma za mtandao. 

Mwakilishi kutoka Tigo Bw. Delphina Msuya akielezea huduma zitolewazo na kampuni ya Airtel wakati wa mafunzo kwa wadau wa huduma za mtandao.


Mwakilishi kutoka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Bw. Deogratius Urassa akielezea huduma mbalimbali zitolewazo na TTCL wakati wa mafunzo kwa wadau wa huduma za mtandao.

Mwakilishi kutoka Kampuni ya Simu ya Vodacom Bw. Athumani Ngoma akielezea huduma mbalimbali zitolewazo na Vodacom wakati wa mafunzo kwa wadau wa huduma za mtandao.

Mwakilishi kutoka Kampuni ya Simu ya Halotel Bw. Steven Komu (Kulia) akifafanua juu ya huduma zitolewazo na Halotel wakati wa semina ya wadau wa huduma za mtandao.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.