• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wadau Jijini Dodoma watakiwa kutumia rasilimali vizuri kwa maslahi ya Mtoto

Imewekwa tarehe: June 15th, 2019

Wadau wa mapambano dhidi ya ukatili kwa watoto katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutumia vizuri rasilimali zilizopo kwa manufaa ya ulinzi na ukuaji wa mtoto.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la KISEDET, Nino Tragni ofisini kwake muda mfupi kabla ya kuanza kwa jukwaa la watoto la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na wadau na kudhaminiwa na KISEDET leo.

Tragni alisema “jamii inatakiwa kuwa ‘pro active’ kutumia vizuri rasilimali kidogo zilizopo kwa manufaa ya ukuaji wa watoto”. Alishauri kuwa maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yafanyike katika maeneo ambayo watoto wanatoka kuliko kupelekwa maeneo ambayo yana muingiliano wa shughuli nyingine za kijamii na uchumi jambo linaloondoa umakini wa maadhimisho hayo.

Akiongelea vitendo vya ukatili kwa watoto, Mkurugenzi huyo aliitaka jamii kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili.  “Ni muhimu kutoa elimu hii katika shule kwa watoto wenyewe na walimu pia. Elimu hiyo iwawezeshe walimu kugundua viashiria vya ukatili kwa watoto mapema kabla havijatokea na kusababisha usumbufu kwa watoto”, alisema Tragni.

Mkurugenzi huyo aliipongeza serikali kwa kuajiri maafisa ustawi wa jamii wengi katika maeneo mbalimbali. “Serikali ipeleke fedha katika idara ya ustawi wa jamii na elimu ili maafisa hao waweze kutekeleza majukumu yao vizuri” alisisitiza Tragni. Aidha, aliwashauri maafisa ustawi wa jamii kutoka ofisini na kutembelea makao ya watoto na maeneo mengine ili kujadili changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.  

Nae mjumbe wa jukwaa la watoto katika Halmashauri ya jiji la Dodoma, Kaisi Omary alishauri kuwa watoto wasiteswe na kunyanyaswa. “Mimi nachowashauri msiwatese hawa watoto sababu watoto ni wakwetu sote. Tuwapende, tuwalinde tukiwaelekeza wanafuata kile tunachotaka. Pia waepuke makundi mabaya na matumizi ya vilevi kama kunywa pombe na kuvuta bangi. Kilevi kinamuaribu saikolojia na akili yake, anakuwa kila muda anawaza pombe na kuiba” alisema Omary. Akiongelea siku ya mtoto wa Afrika alisema kuwa siku hiyo inawapa fursa watoto kutaja mambo yanayowakera ili jamii iweze kuyatatua.

Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika mwaka 2019, yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Mtoto ni msingi wa Taifa endelevu, tumtunze, tumlinde na kumuendeleza”. Maadhimisho hayo yanatanguliwa na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na jukwaa la watoto linalofanyika katika makao ya watoto KISEDET na kilele chake kitafanyika kesho katika shule ya msingi Chang’ombe iliyopo Kata ya Chang’ombe jijini hapa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.