• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Wafanyabiashara Dodoma, acheni kuvamia maeneo yasiyo rasmi” - Afisa Masoko

Imewekwa tarehe: January 29th, 2020

Afisa Masoko wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, James Yuna (pichani juu) amewataka wafanyabiashara jijini hapa kuhakikisha wanayatumia maeneo ya masoko yaliyotengwa na Halmashauri ya Jiji ipasavyo ili kuweza kuepukana na athari zinazoweza kujitokeza pindi wanapovamia maeneo yasiyo rasmi na kuyarasimisha kwa kufanyia biashara zao.

Yuna ameyasema hayo wakati  akihojiwa  kwenye kituo cha redio cha Dodoma FM katika kipindi cha  Dodoma live, ambapo ametoa ufafanuzi juu ya masoko yaliyopo katika maeneo ya Jiji la Dodoma na namna  ambavyo wafanyabiashara  hawayatumii na badala yake kupanga bidhaa zao barabarani hali inayohatarisha usalama wao na bidhaa pia.

Afisa masoko huyo alisema Dodoma ni moja kati ya Halmashauri zenye miundombinu mizuri hasa upande wa masoko, ambapo karibia kila eneo kuna soko ambalo wafanyabiashara wanaweza kulitumia katika kujipatia kipato lakini hali imekuwa tofauti kwani badala ya wananchi kufuata mahitaji sokoni mahitaji yamekuwa yakiwafuata barabarani.

“Jiji la Dodoma lina Kata 41, mpango wa Jiji kila Kata inapaswa kuwa na soko na ni Kata chache ambazo bado hazina, tayari Halmashauri ilishatenga maeneo hayo, katikati ya mji tuna masoko 12 ambayo yanafanya vizuri na kuhudumia wateja wengi ikiwemo soko la Bonanza linalohudumia wananchi kwa upande wa matunda, mbogamboga, mahindi mabichi na samaki wabichi.

“Pia tunalo soko la Majengo ambalo ndio kongwe zaidi na mengineyo ambayo yanafanya kazi chini ya usimamizi wa ofisi ya Mkurugenzi,  ambapo mfanyabiashara anatakiwa kuandika barua ya kuomba eneo na kisha atapatiwa majibu kama eneo lipo na atapewa, lakini kumekuwa na changamoto kubwa ya maeneo rasmi ya masoko kutokutumiwa na badala yake wanatumia kupanga biashara zao barabarani na kuathiri utendaji kazi wa maeneo hayo,” alisema Yuna.

Aidha ametoa ufafanuzi juu ya upangishaji wa vibanda vya biashara ambapo wengi wamekuwa wakifanya udalali na kuwatoza hela kubwa tofauti na ile iliyopangwa na Halmashauri, ametoa onyo kwa wale wote wenye tabia hiyo kuacha mara moja kwani kufanya vitendo hivyo ni kinyume na taratibu na endapo watabainika watachukuliwa  hatua za kisheria.

“Ukipata eneo la kufanyia biashara fanya wewe mwenyewe na endapo utashindwa toa taarifa kwa mamlaka husika na libaki kuwa wazi ili  mfanyabiashara mwingine anayehitaji kulitumia apatikane na apangishwe.

“Wafanyabiashara pia hakikisheni mnatoa taarifa sehemu husika endapo mtabaini kuna vitendo hivi vya udalali vinaendelea katika masoko yenu ili sisi tupate kuyafahamu, lakini endapo ninyi mtashindwa kuwa wakweli mnaokumbana na adha hii itakuwa ngumu kupatiwa msaada wa haraka,” alisema Afisa Masoko huyo.

Aidha alitoa wito kwa wafanyabiashara wote kuhakikisha wanayatumia masoko yaliyoko kwenye maeneo yao na kusisitiza kuwa  wanaendelea kutoa elimu juu ya dhana ya utafutaji, na kuwahimiza kila mtu aendelee kuwajibika katika eneo lake na kuepukana na uvamizi wa maeneo yasiyo rasmi.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.