• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wafanyabiashara Dodoma washauriwa kujiandikisha orodha ya wapiga kura

Imewekwa tarehe: October 15th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Wafanyabiashara wameshauriwa kutumia haki yao ya msingi ya kikatiba kupiga kura kwa kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili waweze kupiga kura na kuwachagua viongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa Kidia Vision Hotel, William Moshi  alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa wafanyabiashara kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa nje ya hoteli yake.

Moshi alisema kuwa anawahamasisha wananchi wa halmashauri ya jiji la Dodoma kujitokeza kushiriki zoezi la kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura. Kupiga kura ni haki ya msingi ya kikatiba. Wananchi watumie fursa hiyo kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa ili kuepukana na madhara yote yatakayojitokeza pindi wasipojiandikisha katika orodha ya wapiga kura na kushindwa kuwachagua viongozi bora.

“Nawasihi wakazi wote na wafanyabiashara wa Jiji la Dodoma na wakazi wengine wote, kujitokeza kwa wingi na kujiandikisha kutumia haki yao ya msingi ya kikatiba, kuchagua viongozi wao kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa. Hakuna mtu mwingine anayeweza kukuchagulia wewe kiongozi anaefaa bali ni wewe mwenyewe mkazi wa mtaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla tujitokeze kwa wingi tukajiandikishe kwenye orodha ya wapiga kura” alisema Moshi.

Akiongelea uchaguzi wa viongozi bora, alisema kuwa wanachaguliwa na watu wenyewe kwa ajili ya maendeleo yao. “Hakuna mtu mwingine mwenye wajibu wa kukuchagulia kiongozi, bali ni wewe mfanyabiashara, mwananchi na mkazi wa kawaida kutumia nafasi hii ya kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ili uweze kuchagua kiongozi anaekufaa kwa ajili ya maendeleo yako na taifa lako” alisisitiza Moshi.

Akiongelea madhara ya mtu kupoteza sifa ya kuwa mpiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa alisema kuwa ni kutojiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura. “Madhara ambayo yanatokana na kutojitokeza kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura, kwanza, hutoweza kupiga kura na kama hutoweza kupiga kura utakuwa umepoteza haki yako ya msingi ndani ya miaka mitano ya kumchagua kiongozi ambaye unaona anafaa. Madhara mengine utabaki unalalamika kuwa kiongozi ambaye yupo madarakani hafai, wakati ulipewa nafasi hukuitumia. Halmashauri ya Jiji la Dodoma takribani wiki mbili, tatu inatangaza kwenye magari ya matangazo wananchi wajitokeze kujiandikisha” alisisitiza Moshi.

Pia aliwashauri wananchi wenye sifa na vigezo vya kupiga kura na kuandikishwa kwenye orodha ya wapiga kura wajitokeze kwa wingi kabla zoezi halijaisha ili waweze kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. “Mpiga kura anapaswa awe ametimiza umri wa mika 18 na kundelea, anatakiwa awe na akili timamu ili aweze kutambua ni kiongozi gani anayeweza na kufaa kumuongoza, kiongozi gani anaweza kufaa kuwa chachu ya maendeleo katika nchi hii, awe mkazi wa mtaa husika, awe amejiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika mtaa husika na awe ni raia wa Tanzania. ‘Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi’

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.