• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wahitimu chuo cha Mipango watakiwa kuchangamkia fursa za zabuni za Umma

Imewekwa tarehe: December 16th, 2022

SERIKALI imewataka wahitimu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) kuchangamkia fursa ya upendeleo inayotolewa na sheria ya manunuzi inayozitaka taasisi zote za Serikali kutenga asilimia 30 ya bajeti zao za manunuzi ya mwaka kwa ajili ya makundi maalum katika jamii wakiwemo vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu.

Rai hiyo imetolewa jijini Mwanza na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Jenifa Omolo ambaye alimwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika mahafali ya 36 ya Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini duru ya pili katika Kituo cha Mafunzo cha Kanda ya Ziwa, jijini Mwanza.

Omolo alieleza kuwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya Bajeti kuu ya Serikali hutumika kwenye manunuzi mbalimbali ya bidhaa, huduma na kandarasi za ujenzi na hivyo ni vema wakachangamkia fursa hiyo.

‘‘Bajeti ya manunuzi kwa mwaka huu wa fedha ni takribani Sh. trilioni 32, ambapo asilimia 30 ya kiasi hiki ni takribani sh. trilioni 9.78 ambazo zinapaswa kutengewa makundi haya maalum. Hivyo, niwaase vijana wetu kujiunga katika makundi na kuyasajili rasmi ili yatambulike kuweza kunufaika na fursa hiyo’’, alisema Omolo.

Alifafanua kuwa Serikali iko tayari kusaidia vijana wenye mawazo chanya ya kibiashara kutimiza malengo yao jambo la msingi ni kujiunga kwenye vikundi vyenye lengo la aina moja ili iwe rahisi kukabiliana na changamoto ya mtaji mdogo kwa kushirikiana na wenzako katika kikundi kuliko mtu akiwa peke yake.

Omolo aliwaasa wahitimu kuwa na moyo wa uthubutu na kuyafanyia upembuzi yakinifu mawazo yao ya biashara, kuyaandalia mpango wa biashara na kuyatekeleza kwa ufanisi bila kukata tamaa kwani ulimwengu wa leo unahitaji moyo wa kupenda kuendelea kujifunza na zaidi kuwa wabunifu.

Alitoa rai kwa wazazi na walezi kuiunga mkono Serikali kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wahitimu hao kwa kuwawezesha watakaokuwa na mawazo ya kibiashara kupata mitaji ya kuanzisha miradi yao ya biashara.

‘‘Serikali kwa upande wake itaendelea na agenda yake ya kuboresha mazingira ya upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya vijana kupitia mikopo inayotolewa na mamlaka za serikali za mitaa’’ alisema Omolo.

Pia Omolo alizitaka Bodi za taasisi zote za umma kuzisimamia vizuri taasisi zinazotekeleza miradi ya ujenzi ili thamani ya fedha ionekane kwani palipo na usimamizi mzuri wa miradi ya ujenzi Serikali haitasita kutoa fedha za maendeleo.

Aidha, alitoa rai kwa taasisi nyingine za elimu ya juu na kati na ikiwezekana shule za sekondari kuiga mfano wa chuo hicho wa kuwaandaa wataalamu kuwa mahiri na weledi kwa kutumia mfumo unaohusisha nadharia na vitendo, vilevile kozi zenye moduli ya masuala ya ujasiriamali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho, Prof. Martha Qorro, ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za maendeleo kuwezesha chuo hicho kutekeleza kwa ufanisi mradi wa upanuzi wa chuo.

Pia alisisitiza kuwa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho litaendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kukisimamia chuo hicho kuboresha mazingira yake na miundombinu huku likitanguliza maslahi mapana ya Taifa ili kukiwezesha chuo kupata mafanikio zaidi.

Naye Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo ya Vijijini Prof. Hozen Mayaya, alisema kuwa wahitimu hao wamefundishwa na wamefuzu kuweza kuingia katika kutumikia Taifa wakiwa na maarifa na ujuzi stahiki katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Alisema kuwa chuo hicho kimejidhatiti katika kuwaandaa wataalamu wenye weledi wa kutosha katika fani za mipango ya maendeleo, bali pia kutoa huduma iliyo bora kwa wakati na inayokidhi matakwa ya wadau.

Aliishukuru Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuendelea kukiwezesha Chuo kupata miundombinu ya msingi ambayo ni bora na ya kisasa ikiwemo majengo yaliyowekewa mawe ya msingi na uzinduzi.

Jumla ya wahitimu 2691 wakiwemo wanawake 1491 na wanaume 1200 wamehitimu mafunzo yao na kutunukiwa Astashahada Stashahada na Shahada ya kwanza kwa wahitimu wa Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini katika programu 3 kwenye mahafali ya 36 ya Chuo duru ya pili katika Kituo cha Mafunzo Kanda ya Ziwa Mwanza.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.