• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wahusika ubadhilifu, miradi yenye kasoro kukiona

Imewekwa tarehe: October 14th, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameitaka Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kifanyia kazi taarifa ya Mbionza Mwenge wa Uhuru na kuwachukulia hatua stahiki wale watakaobainika kuhusika na ubadhilifu katika miradi iliyotajwa kuwa na kasoro.

Mhe. Rais Samia, amesema hayo leo tarehe 14 Oktoba, 2021 wakati akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru, Kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere na Wiki ya Vijana yaliyofanyika katika viwanja vya Magufuli wilayani Chato Mkoani Geita.

Amesema haiwezekani kufikia maendeleo kama taifa litaendelea kkuwa na vitendo va rushwa na ufisadi, kwani vitengo hivyo ni chanzo cha ukiukwaji wa haki za wananchi, kuwepo kwa mikataba mibovu na ukiukwaji wa taratibu za ujenzi katika miradi ya maendeleo.

Aidha, Mhe. Rais Samia amesema amekuwa akijiuliza kwa nini viongozi wa maeneo ambayo miradi iliyokutwa na dosari ikiwa ni pamoja na Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Maofisa TAKUKURU na viongozi wa vyombo vya ulinzi ya usalama wapo lakini wanasubiri mpaka wakati wa mbio za Mwenge wa Uhudu zipite ndipo wabaini dosari za miradi hiyo.

Mhe. Rais Samia ametoa tahadhari kwa miradi inayokwenda kutekelezwa kwenye Mpango wa Maendeleo kwa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 kuwa lisijitokeze suala la ubadhilifu na kuwa atasimama imara kufuatilia utekelezaji wa miradi hiyo na miradi mingine.

Pia, Mhe. Rais Samia amewataka viongozi katika maeneo utakapopita Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 kuhakikisha idadi ya miradi yenye dosari inapungua.

Akizungumza juu ya kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere, amesema Serikali itaendelea kumuenzi Baba wa Taifa, kutokana na ujasiri aliokuwa nao ukiwemo ushupavu wa kuitumikia nchi yake.

Kuhusu sekta ya afya, Mhe. Rais Samia amesema bado hali sio nzuri kutokana na kuongezeka kwa maradhi yasio ya kuambukiza yakiwemo ya shinikizo la damu, Kisukari, Malaria pamoja na janga la UVIKO 19, jambo ambalo ni vyema kwa vijana wa Tanzania kuendelea kuchukua tahadhari ya maradhi hayo.

Mhe. Rais Samia, amewataka wnanchi kujikinga na UVIKO 19 kwa kuona umuhimu wa kuchanja kwani Serikali tayari imeshasambaza chanjo na kuwaasa vijana kuacha kutumia dawa za kulevya kutokana na athari zake kwa afya.

Mwenge huo wa Uhuru umetembelea, kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 1,067 yenye thamani ya Zaidi ya Shilingi Trilioni 1.2 kutoka sekta za maji, nishati, afya, kilimo, uvuvi, mifugo na miundombinu.

Mapema alipowasili Wilayani Chato, Mhe. Rais Samia alizuri na kuweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli nyumbani kwako Chato mkoani Geita.

Maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru zimefanyika Wilaya ya Chato Mkoani Geita ili kumuenzi aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.