• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wajasiriamali Jiji la Dodoma wahimizwa kurasimisha biashara zao

Imewekwa tarehe: November 13th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

WAJASILIAMALI  katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehimizwa kurasimisha biashara zao kwa lengo la kuwa na wigo mkubwa wa kuweza kukopa katika taasisi za kifedha kwa sababu watakuwa wanatambulika kwa mujibu wa sheria.

Hayo yalisemwa na Katibu Mtendaji wa Shirika Kakute Projects, Livinus Manyanga alipokuwa akizungumza na wanufaika wa mradi wa nishati jadidifu, wadau wa serikali, viongozi wa sekta ya biashara na wazalishaji wa teknolojia katika mkutano wa wadau wa mradi wa nishati jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji uliofanyika katika ukumbi wa Maktaba ya Mkoa uliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

“Tumejaribu kufanya kazi kwa karibu sana na vile vikundi ambavyo vimekopeshwa mikopo na halmashauri tofauti na hii misaada ambayo tumeitoa sisi, inaonesha wazi kwamba changamoto namba moja ni kwamba, mjasiriamali mdogo mpaka aweze kurasimisha biashara yake ni hatua ndefu na hawapendi kuchukua hatua ndefu kiasi hicho. Pia nidhamu ya matumizi ya pesa, kujua hii pesa imetoka wapi na inatakiwa kupelekwa wapi inakuwa ni ngumu kidogo. Tunazidi kusisitiza, uwekaji wa kumbukumbu, mpango wa biashara na kurasimisha biashara ni vitu vya msingi sana” alisisitiza Manyanga.

Akiongelea suala la teknolojia katika mradi, alisema kuwa wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwafikia walengwa na imesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha biashara zao. “Teknolojia imetengenezwa vizuri na inaonesha muelekeo wa kuwaongezea uzalishaji na pia kuboresha maisha yao kwa ujumla” alisema Manyanga.

Kuhusu suala la wadau wa kifedha, alisema mradi unashirikiana na taasisi mbalimbali za kifedha ili kuwasaidia wajasiriamali wadogo wadogo katika kata zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuboresha miradi na kuimarisha usambazaji wa teknolojia. “Mradi unalenga kuwashirikisha wajasiriamali na wadau wa fedha kama SACCOS, VICOBA pamoja na Benki.  Pamoja na mafunzo tuliyowapatia wajasiriamali waliopo maeneo ya pembezoni, uelewa wao ni wa taratibu, wanafahamu kila kitu lakini kutekeleza ni taratibu” alisema Manyanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa DOM Energy Solutions and Designing Ltd, Anthony Machai, ambae ni msambazaji wa teknolojia katika mradi huu alipongeza juhudi za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kampeni ya kutokomeza matumizi ya nishati chafu na hivyo, kumuunga mkono katika kusambaza teknolojia ambayo ni rahisi kwa wajasiriamali wa baadhi ya kata zilizopo jijini Dodoma kwa kushirikiana na Kakute Projects.

“Tunajishughulisha na ufungaji wa mitambo ya ‘solar’ mbalimbali katika Jiji la Dodoma na Tanzania nzima. Ukiangalia kwa sasahivi pia rais wetu yupo kwenye mchakato wa kuhakikisha wananchi kwa asilimia kubwa tunatumia nishati safi ambayo inatunza mazingira. Na sisi kama wadau wa nishati, tunampongeza kwa jitihada nyingi sana anazozifanya kutafuta wafadhili wengi watakaoiwezesha jamii yetu kupata nishati hii ambayo ni rahisi na kila mmoja anaweza akamudu” alisema Machai.

Kwa upande wake mjasiriamali, Lucas Japhet ameipongeza serikali kwa kuwaletea wadau ambao wamekuwa ni chachu kubwa sana katika kukuza biasahara zao na kuyafikia malengo kwa teknolojia nzuri walizowekewa. “Nimefungiwa mtambo wa ‘solar’ na umenirahisishia mimi kufanyakazi zangu kwa uhuru zaidi na kwa wepesi zaidi na mpaka sasahivi kuna mafanikio mazuri nimeyafikia na kikubwa ninafanya kazi kwa urahisi zaidi bila shida yoyote. Niishukuru serikali yetu ya Tanzania kwa kutuletea wadau kama hawa wanaotuwezesha sisi wajasiriamali kupata nishati na hata kwa jamii pia” alisema Japhet.

Mradi wa nishati jadidifu kwa matumizi ya uzalishaji Dodoma ulianzishwa mwaka 2022 na kuweza kuzifikia kata tano ambazo ni Mbalawala, Chihanga, Hombolo Makulu, Mnadani pamoja na Ipala na kuwafikia wajasiriamali 15 ambao walipatiwa mitambo ya kuendesha biashara zao za uzalishaji. Pia ulilenga kuimarisha na kuboresha miradi ya wajasiriamali wa pembezoni iwe na tija zaidi kwa kuunda ushirikiano kati  ya wasambazaji wa suluhisho za teknolojia ya nishati jadidifu na kujenga msingi wa maendeleo endelevu kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ngazi ya kata na wadau wengine wa maendeleo.

MWISHO




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.