• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wajasiriamali msilalamike, tafuteni wanufaika - SIDO

Imewekwa tarehe: August 7th, 2020

WAJASIRIAMALI nchini wamekumbushwa kuwa wanawajibu wa kuwatafuta wanufaika wa bidhaa zao sehemu mbalimbali ili waweze nunua bidhaa hizo tofauti na dhana iliyozoeleka ya kukaa wakisubiri na kulalamikia soko.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa uendeshaji biashara wa Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Dodoma, Crispin Kapinga alipokuwa akielezea wajibu wa wajasiriamali katika kujitangaza na kutafuta masoko katika banda la SIDO kwenye maonesho ya Nanenane, Nzuguni jijini Dodoma.

Kapinga alisema “kilio kikubwa cha wajasiriamali ni soko, sasa tumekuja kuwaonesha kuwa soko siyo tatizo. Tatizo ni sisi wenyewe wajasiriamali kwa sababu tunataka wateja watufikie tulipo kitu ambacho hakiwezekaniki. Katika dunia ya sasa, watu wanatakiwa kulifuata soko lilipo. Kati ya bidhaa na mteja, anaanza mteja ndipo inatengenezwa bidhaa kulingana na matakwa ya mteja”.

Alisema kuwa tatizo lililopo ni wajasiriamali kuamua kutengeneza bidhaa baada ya kuona rafiki yake anaitengeneza na kuuza bila kuangalia ukubwa wa soko la bidhaa hizo.

Katika maonesho haya wajasiriamali wamejifunza kile tulichowafundisha darasani na kukiona katika uhalisia wake, aliongeza.

Akiongelea ushiriki wa wajasiriamali katika maonesho ya Nanenane, alisema “huku wamekuja kutangaza bidhaa zao, wamepewa ushauri na kukosolewa juu ya kutengeneza na kuboresha bidhaa zao kutoka kwa watu waliotembelea banda letu, jambo ambalo ni jema katika uboreshaji wa huduma na bidhaa zao”.

Afisa huyo aliwataka wajasiriamali kuacha kulalamika na kuamini katika fedha pekee. Aliwakumbusha kuwa fedha ni kitu cha pili, baada ya kuwa na maono na mawazo sahihi yanayoweza kuwasaidia kutengeneza bidhaa nzuri zinazoweza kushindana na bidhaa nyingine katika soko.

Kuhusu mchango wa SIDO kwa wajasiriamali, Kapinga alisema kuwa, SIDO Mkoa wa Dodoma uliwapatia mafunzo ya kutengeneza bidhaa na jinsi ya kuziingiza sokoni, ushauri wa kibiashara na kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwezo bidhaa za ngozi.

Aidha, SIDO imewakutanisha wajasiriamali na wadau wanaohusika na vifungashio na kupata suluhu ya changamoto ya vifungashio iliyokuwa ikiwakabili wajasiriamali wengi.

Maonesho ya Nanenane mwaka 2020 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kwa maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, chagua viongozi bora 2020”





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.