• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wajumbe wa baraza la wafanyakazi wapitia rasimu ya bajeti 2025/26

Imewekwa tarehe: January 20th, 2025

Wajumbe wa baraza la wafanyakazi wapitia rasimu ya bajeti 2025/26

Na. Coletha Charles, DODOMA

Baraza la Wafanyakazi Halmashauri ya Jiji la Dodoma limetakiwa kupitia mapendekezo ya rasimu ya makisio ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 kwa kutoa mchango wa mawazo kwa lengo la kuboresha nyaraka za bajeti kwa kutengeneza mazingira rafiki kwa wageni na wenyeji wa Mkoa wa Dodoma.


Hayo yalisema na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi pia Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, katika ukumbi wa mikutano wa halmshauri hilo, alipokuwa akifungua kikao kwa ajili ya kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 pamoja na mpango wa makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026.


Alisema kuwa mawazo hayo ni moja ya utekelezaji wa kila mtu kuifanya Dodoma iwe kimbilio la watu wengi duniani kwa kutamani kufika na kuwekeza. “Ninaomba mtoe mawazo yenu tunajua mpo wengi wenye uwezo katika maeneo yenu, tumieni fursa ya kuja kutoa mchango wa nini kifanyike na kwa thamani gani. Miongoni mwa wengi na nyinyi mmebahatika kuwa wajumbe wa baraza hili, sasa tutumie hii bahati na neema ya mwenyezi mungu, kuwafanya nyie kuwa wajumbe muweze kutoa mchango wenu wa dhati ili unapoona Dodoma inabadilika uweze kujivunia kwamba hii ilikuwa sehemu ya mchango wangu” alisema Dkt. Sagamiko.


Mwenyekiti wa baraza hilo, aliongeza kuwa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/26 ni bajeti ya kimkakati zaidi kwa ajili ya kuboresha mazingira na kumaliza miradi vipolo, ambapo mwaka fedha 2026/27, fedha itakayopelekwa kwenye kata inaweza kuongezeka zaidi na kipaumbele kikubwa ni sehemu za kutolea huduma na walengwa ni watumishi wa umma katika kuboreshewa mazigira yao.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prosper Kyaruzi, alibainisha kuwa kikao hiko kilikuwa maalum kwa ajili ya kupitisha rasimu ya makadilio ya kujadili bajeti kabla haijaenda kwenye baraza la madiwani kwa ajili ya kupitishwa.

Alisema kuwa baraza hilo lina umuhimu mkubwa kwa wawakilishi wa wafanayakazi kwa kujadili na kuangalia vipaumbele ambavyo vimewekwa na idara moja baada ya nyingine kwa kukubaliana navyo, kufanyiwa kazi na badae bajeti inapitishwa kwa kuangalia mstakabali na masilahi ya wafanyakazi. “Kwanza tumempokea mkurugenzi mpya kwenye kikao cha kwanza cha baraza la wafanyakazi, Dkt. Frederick Sagamiko, amekuwa na sisi kuanzia mwanzo wa kikao hadi mwisho. Nimefurahi sana kwa upande wa sisi walimu tunaowakilisha idara ya msingi na sekondari amesema tutakuwa na kikao kwa ajili ya kujadili stahiki mbalimbali za walimu ambazo zilikuwa bado hazijatimizwa. Lakini pia tumeona tuna Mkurugenzi mwajibikaji ambaye anaupendo mkubwa sana” alisema Kyaruzi.


Ikumbukwe kuwa, kwa mwaka wa fedha 2023/24 Halmshauri ya Jiji la Dodoma ilikadiria kutumia jumla ya shilingi bilioni 123.8 kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato, mwaka wa fedha 2024/25 Halmshauri hiyo ilikadiria kutumia jumla ya shilingi bilioni 143.1 kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato na rasimu ya makisio ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 ni jumla ya shilingi bilioni 147.9 kati ya fedha hizo shilingi bilioni 67.3 ni mapato ya ndani, ruzuku ya mishahara shilingi bilioni 65.7, ruzuku ya miradi ya maendeleo shilingi bilioni 11.7 na ruzuku ya matumizi mengineyo shilingi bilioni 3.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.