• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakaguzi wa vifaa tiba na dawa Kanda ya Kati wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu

Imewekwa tarehe: March 10th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAKAGUZI walioteuliwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu na weledi katika kudhibiti ubora na ufanisi wa bidhaa zinazodhibitiwa na TMDA ili kulinda afya za wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Fatuma Mganga alipokuwa akifungua kikao kazi cha wakaguzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wakala wa Majengo Tanzania jijini Dodoma.

Dkt. Mganga alisema “napenda mfahamu kuwa utendaji kazi wowote hupimwa kwa taarifa. Hivyo, mwongozo wa kukasimu madaraka na majukumu umebainishwa wazi kuwa taarifa za utendaji kazi za robo mwaka na taarifa za ufuatiliaji na tathmini ya utendaji kazi za udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa zinazodhibitiwa na TMDA katika soko zinatakiwa kuandaliwa na kutumwa TMDA kupitia viongozi wenu katika ngazi ya halmashauri. Nimatumaini yangu mtafanya kazi kwa weledi na uadilifu mkubwa”.

Katibu Tawala huyo aliwataka washiriki wa mafunzo kutumia mafunzo hayo kuboresha utendaji kazi wao. “Kupitia mafunzo haya mkatatue changamoto zinazojitokeza mara kwa mara na hivyo, kusaidia wakaguzi wa halmashauri kutotumia nguvu nyingi nyakati za kaguzi ambazo husababishwa na kutokutoa elimu kwa wateja. Hivyo, kukinzana na utaratibu wa ukaguzi wa TMDA ambao umejikita zaidi katika kuelimisha na kuwezesha” alisema Dkt. Mganga.

Nae Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kanda ya kati, Sonia Mkumbwa aliwakumbusha wakaguzi hao kutumia sheria, kanuni na miongozo katika utoaji huduma. “Nitoe rai kwa wataalam wote kwenye kada ya Afya kuendelea kufuata sheria, kanuni na miongozo katika utoaji wa huduma. Kwa kuhakikisha bidhaa ambazo wanazitoa wao wenyewe kabla ya kumpa mtu uhakikishe kwamba umeiangalia na inakidhi matakwa ya ubora na usalama ndiyo umpe mtumiaji. Lakini pale utakapopata changamoto yoyote sisi TMDA tupo kwenye kanda nane na taifa kwa ajili ya kutoa msaada. Mfamasia, mtaalam wa maabara na daktari kwenye halmashauri husika ni muwakilishi wa TMDA kama sisi tupo mbali” alisema Mkumbwa.

Akiongelea mafunzo hayo, aliyataja kuwa yanalenga kwenda kutatua changamoto katika maeneo ya kutolea huduma. “Sehemu za kutolea huduma kuna bidhaa zenye ubora tofauti. Mfano bidhaa bandia na bidhaa duni. Kuna bidhaa nyingine tarehe ya kutumika bado ipo vizuri lakini kutokana na uhifadhi wake kuwa duni hakuna feni au kiyoyozi jambo linalosababisha kiwango cha ubora katika bidhaa ile kushuka” alisema Mkumbwa.

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba kanda ya kati inahudumia jumla ya halmashauri 29 ikiwa ilianzishwa mwaka 2012.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.