• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakala wa Misitu (TFS) kukusanya milioni 433/-

Imewekwa tarehe: August 23rd, 2020

WAKALA wa Misitu Tanzania (TFS) wilaya ya Morogoro unakusudia kukusanya kiasi cha Sh milioni 433 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kutokana na tozo za mazao ya misitu ( Forest Royalty) .

Kufuatia tozo hizo , halmashauri ya wilaya ya Morogoro itajipatia asilimia tano na mapato yatakayokusanywa na wakala huo halmashauri hiyo pia itapata fedha za ushuru wa miti pandwa (tozo za mbao).

Kaimu Meneja wa TFS, wilaya ya Morogoro, John Kimario alisema hayo jana katika taarifa yake kwa mkuu wa wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa kabla ya kufungua kikao cha uvunaji wa mazao ya misitu kwenye wilaya hiyo.

Kimario alisema kutokana na changamoto za uvunaji na biashara ya mazao ya misitu, serikali mwaka 2007 iliandaa mwongozo wa uvunaji kwa kuwashirikisha wadau wa misitu na kutolewa mwongozo wa uvunaji endelevu wa kibiashara ya mazao ya misitu yanayovunwa kwenye misitu ya asili.

Alisema madhumuni ya mwongozo huo ni kuhakikisha yanakuwepo matumizi endelevu ya rasilimali za misitu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vijavyo.

Kimario alisema serikali iliunda chombo cha kusimamia uvunaji wa mazao hayo katika kila wilaya na kuwa na kamati ya wilaya ya kusimamia uvunaji wa mazao ya misitu kwa kuzingatia mpango wa uvunaji wa wilaya ulioandaliwa na Wakala huo ngazi ya wilaya.

Alisema uvunaji wa miti ya asili katika maeneo ya msitu wa mataji ( General Lands) utafanyika katika vijiji vya Seregete A na B , Mkulazi , Kidunda , Nyarutanga , Dakawa , Sesenga na Lumbachini .

Kaimu Meneja wa TFS Wilaya hiyo alisema vijiji hivyo nane vinafuata mpango wa uvunaji wa wilaya ambao umeandaliwa na kusimamiwa na wataalamu wa Misitu.

Hata hivyo ,alisema uvunaji katika maeneo ya vijiji kwa miti ya asili ,utavunwa vijiji vinne ambavyo ni Mlilingwa, Matuli , Diguzi na Lulongwe ambavyo vinafuata mpango wa uvunaji wa vijiji na fedha zinazokusanywa na serikali ya kijiji husika na ushuru kwa halmashauri ya wilaya.

Alisema pia kijiji cha Lulongwe hakitakuwemo katika mpango huo kutokana na kutokidhi vigezo vinavyohitajika. Katika hotuba ya ufunguzi wa kikao hicho Mkuu wa wilaya hiyo, Msulwa alisema wilaya ya Morogoro inakabiliwa na tatizo kubwa la uharibifu wa misitu kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu.

Alizitaja baadhi ya shughuli hizo kuwa ni ukataji miti kwa ajili ya kupata nishati , kilimo cha kuhamahama , uchomaji mkaa, upasuaji mbao na ufugaji.

Mkuu huyo wa wilaya alisema moja ya matokeo ya shughuli hizo ni uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji unaosababisha upungufu mkubwa wa maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu, kilimo, mifugo na viwanda.


Chanzo: HabariLeo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.