• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakazi Mkonze watakiwa kushiriki usafi Jumamosi

Imewekwa tarehe: February 5th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAKAZI wa Kata ya Mkonze iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujitokeza kushiriki katika mazoezi ya usafi wa mazingira siku ya Jumamosi ili kuyaweka maeneo yao safi na kuepukana na magonjwa yanayosababishwa na uchafu.

Wito huo ulitolewa na Mlezi wa Kata ya Mkonze, Gratian Mwesiga alipofanya ziara ya kukagua hali ya usafi katika mitaa ya kata hiyo mapema leo.

Mwegasi ambae pia ni Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Jiji la Dodoma alisema kuwa zoezi la usafi katika Kata ya Mkonze halikufanyika kwa kiwango cha kuridhisha.

“Ni kweli tumetembelea baadhi ya mitaa na kukuta maeneo hayajafanyiwa usafi na baadhi ya maeneo ya biashara kufunguliwa. Leo nimelazimika kutoa elimu kwa wananchi. Nimetoa elimu juu ya umuhimu wa usafi wa mazingira mita tano kuzunguka maeneo ya makazi na biashara. Kwa yale maeneo ya biashara ambayo yalikuwa yakiendelea na biashara wakati nakagua saa moja asubuhi, nililazimika pia kukagua leseni zao. Katika ukaguzi huo nimebaini kuwa baadhi hawana leseni na wengine leseni zimeisha muda wake. Nimewaagiza kukata leseni za biashara” alisema Mwesiga.

Alisema kuwa siku ya Jumamosi ni muhimu kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa usafi ni tabia ya kistaarabu. “Wananchi hawatakiwi kupuuzia suala la usafi wa mazingira kwa sababu usafi unatuepusha na magonjwa yanayosababishwa na uchafu. Wananchi wanatakiwa kukumbuka kuwa Dodoma ni makao makuu ya nchi, hatuwezi kuwa na makao makuu ambayo uchafu ni sehemu ya maisha” alisema Mwesiga.

Aidha, alihaidi kufanya kikao na viongozi wa Kata na Mitaa ili kukubaliana mikakati ya kufanya usafi na ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Kwa upande wake mkazi wa Muungano, Yonas Misana alisema kuwa uongozi wa mtaa umekuwa na utaratibu wa kuwataarifu eneo la kufanya usafi wa pamoja ila wiki hii hawakutaarifiwa ndiyo sababu wakaamua kuendelea na biashara zao.

Mlezi wa Kata ya Mkonze Gratian Mwegasi (kulia) ambae pia ni Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma akimhimiza mmoja wa wakazi wa Mkonze kuhusu kufanya usafi kwenye maeneo yanayozunguka biashara, makazi na taasisi leo wakati alipotembelea kata hiyo kukagua shughuli za usafi.

Mfanyabiashara wa kata ya Mkonze aliyekutwa na mpiga picha wetu akifanya usafi kuzunguka eneo la biashara yake kwa hiyari ili kuweka mazingira safi kwa biashara na afya ya wateja.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.