• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakazi wa Jiji Dodoma washauriwa kufuga kisasa

Imewekwa tarehe: August 6th, 2020

WAKAZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujipanga  kwa ufugaji ng’ombe wa kisasa ili waweze kuwahudumia ng’ombe wao vizuri na kupata maziwa mengi.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Gratian Mwesiga (pichani juu) alipokuwa akiongea na waandishi wa habari waliotembelea banda ya mifugo katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika eneo la Nzuguji jijini hapa.

Mwesiga alisema kuwa katika maonesho ya Nanenane mwaka 2020, Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeleta teknolojia rahisi ya ufugaji wa kisasa unaozingatia masharti ya kitaalam kwa lengo la kumpatia tija mfugaji.  

Alisema “ufugaji wa kisasa ni ufugaji unaozingatia utunzaji wa ng’ombe, ulishaji wa ng’ombe, matibabu ya ng’ombe, kalenda ya chanjo kwa ng’ombe izingatiwe, ng’ombe apewe chakula kulingana na uzito wake na kuzingatia ulaji wa chakula cha ziada kama mashudu”.

Wananchi wenye dhamira ya kufuga wanaotembelea banda la Halmashauri ya Jiji wanafundishwa matumizi ya teknolojia na kushauriwa kuzingatia ufugaji wa kisasa wa ndani (zero grazing) ambao unatija zaidi. “Ng’ombe akisafiri umbali mrefu nguvu za kuzalisha maziwa zinapungua sababu chakula badala ya kutumika kuzalisha maziwa kinakuwa kikitumika kwa kutembea huku na kule. Hapa tunatoa elimu ili ng’ombe waweze kutoa maziwa kuanzia lita 15-20. Tunataka tutoke kwenye ufugaji wa asili ambao ng’ombe mmoja anatoa lita 2, huu ni ufugaji ambao hauna tija” alisema Mwesiga.

Akiongelea changamoto ya malisho ya ng’ombe, Afisa Mifugo huyo alisema kuwa katika banda lao elimu ya ulimaji na utunzaji wa malisho inatolewa. “Tuna shamba darasa kwa ajili ya malisho ya mifugo, yapo malisho yanayotokana na mikunde, malisho yanayotokana na nyasi. Nichukue nafasi hii kuwakaribisha wananchi wote wenye nia ya kufuga waje katika banda la mifugo na uvuvi kujionea teknolojia hizo na njia rahisi ya kupanda malisho na utunzaji wake” alisema Mwesiga.

Maonesho ya Nanenane mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Chagua Viongozi bora 2020”

Ng'ombe wakihudumiwa katika banda kwenye maonesho ya Nanenane kutoka kwa wataalam wa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.