• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakazi wa Kata ya Msalato watakiwa kuwajenga watoto kiafya

Imewekwa tarehe: March 8th, 2024

Na. Dennis Gondwe, MSALATO

WAKAZI wa Kata ya Msalato wametakiwa kuwajenga watoto kiafya kwa kuwaandalia lishe bora ili kujenga taifa imara lenye uwezo wa kifikra na uchapaji kazi kwa ajili ya kuliletea maendeleo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Dodoma, Mwl. Neema Majula alipokuwa akiongea wakazi wa Kata ya Msalato kwenye maadhimisho ya kuelekea siku ya wanawake duninia ngazi ya kata yaliyofanyika katika Zahanati ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mwl. Majula alisema “ndugu zangu hali ya lishe ni muhimu sana kwa watoto wetu. Tunapoanza kuwajenga watoto hawa wadogo wawe na lishe bora ndiyo tunajenga kizazi bora cha taifa hili. Tunakuwa tunawekeza kwenye afya na akili za watoto ambao baadae wanapoendelea kukua watakuwa wachapa kazi na wenye uwezo mzuri wa fikra na hivyo, kujiletea maendeleo yao na maendeleo ya taifa letu”.

Akiongelea maadhimisho ya kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani, alisema kuwa yanalenga kumhamasisha mwanamke kuchukua hatua kubwa zaidi ya kimaendeleo kuanzia kisiasa, kijamii hadi kiuchumi.

“Hakuna maendeleo yoyote yatafanyika bila kuwa na afya njema. Tukijenga jamii yenye afya nzuri ndiyo, jamii itaweza kufanya shughuli za maendeleo. Kuanzia kwa watoto wetu ili wasipate udumavu, ili wasipate utapiamlo tukianza kuwanjenga tangu wakiwa wadogo ili wawe na afya njema ndivyo tunajenga kizazi chenye afya njema ambacho kitafanya shughuli za maendeleo” alisema Mwl. Majula.

Lishe ya watoto iende sambamba na lishe ya wababa. “Sasa tujikite kwenye lishe ya watoto wetu, na mimi nipanua kidogo, jamani mpaka lishe ya wababa pia kina mama tufanye. Sisi ndiyo waandaaji wa chakula nyumbani tunahitaji kuanadaa lishe kamili nyumbani, tuweke mchanganyiko wa lishe kamili, wanga, vitamini, protini ukijenga familia ambayo ina afya njema ndiyo itaweza kuwaza mambo ya maendeleo” alisisitiza Mwl. Majula.

Kwa upande wa Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Msalato, Dkt. Abusalami Mpamba alisema kuwa amefurahishwa na ziara hiyo kujionea utekelezaji kwa vitendo zoezi la kuwapikia watoto chakula chenye lishe bora. “Mheshimiwa mgeni rasmi, mtoto ukimlea vizuri akiwa na afya bora ndiyo taifa la kesho. Kwa hiyo, wanawake waliopata elimu leo itaweza kutusaidia kupata watoto bora na watakaosoma vizuri, vichwa vyao vitakuwa na akili nzuri kwa sababu wana afya nzuri. Mimi nikupongeze wewe mgeni rasmi kwa uamizi wako. Umeona tumewaelekeza kwa vitendo jinsi chakula kinavyoandaliwa, umeona na jinsi wanavyopewa na umeshuhudia watoto wanavyokula hii ni faraja sana kwetu” alisema Dkt. Mpamba.

Awali akitoa elimu ya lishe kwa akina mama waliohudhuria kliniki katika zahanati ya msalato Afisa maendeleo ya jamii kata ya msalato, Alfrida Kitandala alisema kuwa lishe bora ni muhimu kwa mtoto kwa sababu inamsaidia kuwa na uwezo mzuri wa kufikiri.

“Kina mama nawahusia juu ya suala la lishe bora, siyo uji tu kwa mtoto bali ni mchanganyiko wa vyakula vingi, kuna matunda, kuna madini na vitamini ambazo ni mboga za majini. Suala la maji ni muhimu kwa watoto wetu, lakini pia kuna vyakula vya mafuta kama karanga na mafuta tunayotumia. Hivyo, tujitahidi sana kuzingatia lishe kwa watoto wetu ili iwasaidie hata kufikiria kwao shuleni na katika maisha ya kawaida” alisema Chitandala.

Nae mzazi, Jailes Felix alishukuru kwa elimu waliyopewa juu ya lishe kwa watoto. “Nilikuwa namtania Afisa Afya wa kata kwamba zoezi hili ziwe endelevu lituhamasishe tuwe tunakuja kliniki mara kwa mara, maana kina mama wengine kuja kliniki huwa ni nadra sana. Hivyo, Mungu azidi kuwabariki nina hakika tumeelewa sana kile tulichofundishwa leo na tunakwedna kufanyia kazi” alisema Felix.

Maadhimisho ya siku ya wanawake Kata ya Msalato yalifanyika kwa kutoa elimu ya lishe bora kwa wanawake na hamasa ya kujishughulisha yakifanyika katika Zahanati ya Msalato inayozungukwa na mitaa sita ikikadiriwa kuhudumia watu 11,000.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.