• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakulima watumieni wataalam kutatua changamoto zenu - DC Mkanachi

Imewekwa tarehe: August 6th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAKULIMA na wafugaji wa mikoa ya Dodoma na Singida wametakiwa kuwa wepesi kuwatafuta wataalam ili watatuliwe changamoto zinazowakabili katika kuleta tija kwenye shughuli zao.

Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara ya kutembelea mabanda ya maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.

Dkt. Mkanachi alisema “wito wangu kwa wakulima na wafugaji hawajawa wepesi kutoka kuwafuata wataalam wa kilimo na mifugo ili wawatatulie changamoto zao. Mtazamo huu lazima tuubadilishe, wakulima na wafugaji lazima watoke kuwatafuta wataalam ili kuleta tija katika mazao ya kilimo na mifugo”.

Mgeni rasmi huyo alionesha kuridhishwa na maandalizi ya maonesho ya Nanenane mwaka 2022. Mkanachi alisema kuwa maonesho ni mazuri na mazao yanaonekana kuhudumiwa vizuri. “Ndugu zangu, changamoto iliyopo ni ukitoka ukaenda pembezoni kidogo hali ni tofauti. Tuliyoyaona hapa kwenye maonesho yanaweza kuleta mapinduzi makubwa ya kilimo. Pembejeo tulizoziona kwenye maeneo zionekane kwa wananchi” alisisitiza Dkt. Mkanachi.

Akiongelea Sensa ya watu na makazi, Mkuu huyo wa Wilaya ya Kondoa alisema kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kuwa vipaza sauti kuelezea umuhimu wa Sensa ya watu na makazi. “Tarehe 23 Agosti, itafanyika Sensa ya sita ya watu na makazi. Waandishi wa habari muwe vipaza sauti ili wananchi wahamasike kuhesabiwa. Sensa hiyo ni ya kihistoria na itakuwa ni Sensa ya sita kufanyika nchini” alisema Dkt. Mkanachi.

Mwananchi aliyetembelea maonesho ya shughuli za wakulima na wafugaji katika viwanja vya Nzuguni, Mwanaisha Juma alisema kuwa yupo tayari kuhesabiwa. “Kuhesabiwa kwani ni nini hadi nisiwe tayari. Kila siku wakubwa wetu tunawaona wakielezea umuhimu wa Sensa ya watu na makazi, lazima nihesabiwe. Nawashauri na watu wengine wote kuhesabiwa ili kuisaidia serikali kufikia kile inachotaka” alisema Mwanaisha.

Maonesho ya shughuli za kilimo na mifugo mwaka 2022 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Agenda 10/30: kilimo ni biashara, shiriki kuhesabiwa kwa mipango bora ya kilimo, mifugo na uvuvi”.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.