• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakurugenzi watakiwa kutenga fedha kwaajili ya ununuzi wa vifaa vya TEHAMA

Imewekwa tarehe: February 5th, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WAKURUGENZI wa mamlaka za serikali za mitaa wametakiwa kutenga fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya kununua vifaa vya Tehama kwa ajili ya kuwezesha mfumo wa ufundishaji mubashara unaomuwezesha mwalimu mmoja kufundisha zaidi ya shule mmoja kwa wakati mmoja.

Agizo hilo lilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohammed Mchengerwa alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa majaribio ya ufundishaji mubashara uliofanyika katika Shule ya Sekondari Dodoma.

“Kama nilivyosema, tuna uhaba wa walimu takribani 271,028 nchi nzima. Mnaweza kuona uhaba huu ni mkubwa sana na jitihada za Rais wetu ambae ametupa maono ya kwenda kupunguza uhaba wa walimu na ndio maana tumekuja na mfumo huu wa Tehama wa ufundishaji mubashara. Nichukue fursa hii kuwapongeza walimu wote wa Kibaha Sekondari na Dodoma Sekondari. Nimejionea majaribio na nimeridhika na kwajitihada hizi sasa niwaelekeze wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kwenye bajeti ijayo 2024/2025 wahakikishe wanatenga fedha za kutosha ili tuanze mchakato wa kununua vifaa hivi vya Tehama. Kwa wakuu wa mikoa na makatibu tawala wa mikoa kuhakikisha wanateua shule maalum ambazo zitakuwa nguzo kwaajili ya kusambaza mfumo huu wa Tehama” alisema Mchengerwa.

Aidha, alimuelekeza Katibu Mkuu Tamisemi kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ili kuhakikisha mfumo huo unaenea nchi nzima ifikapi mwezi Desemba, 2025. “Majaribio haya tunaita ufundishaji mubashara ambayo ni moja ya jitihada za serikali ya awamu ya sita kwa kwenda kupunguza uhaba wa walimu katika maeneo yote nchini” alisema Mchengerwa.

Akiongelea changamoto ya uhaba wa walimu, alisema kuwa Tamisemi ililiangalia jambo hilo la uhaba wa walimu katika nyanja mbili na kugundua uhaba wa walimu bado ni mkubwa sana. “Kwakuwa tumekwenda kwenye majaribio ya Tehama na tunajua yatakuwa na changamoto nyingi sana ikiwemo uhaba wa vifaa, lakini hapa kipekee niwapongeze sana kwa wale ambao walijitolea kutoa vifaa mbalimbali kwasababu jitihada hizi za Rais, Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kwamba tunapunguza changamoto ya walimu lakini pia kuongeza ufahamu kwa vijana wetu wanaosoma shule za awali, msingi na sekondari” alisema Mchengerwa.

Kwa upande wa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma, Faudhia Said alisema kuwa mfumo huo wa ufundishaji ni mzuri kwasababu utakuwa unasaidia katika zile shule ambazo zina upungufu wa walimu na kuongeza ufaulu kote nchini.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.