• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakurugenzi watakiwa kuwa makini usimamizi wa fedha

Imewekwa tarehe: January 20th, 2020

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza usimamizi katika fedha zinazokusanywa kupitia mfumo wa kielektroniki ili kuondoa kero zinazowakabili wananchi.

Nyamhanga ametoa maelekezo hayo alipokuwa akifungua semina na mkutano mkuu wa wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa wataalamu wa Tanzania na Osaka Japan (TOA) unaofanyika jijini Dodoma.

Amesema wakurugenzi hao wanatakiwa kuongeza usimamizi wa ukusanyaji wa mapato kupitia mifumo ya kidijitali ili kusaidia kuongeza mapato ya ndani.

“Msimamie hizi fedha ili zileta tija katika kuboresha maeneo mbalimbali ya nchi ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakikabiliwa na changamoto nyingi za huduma kama afya, maji pamoja na elimu,” alisema Nyamhanga.

Aidha, amewataka wakurugenzi hao kuhakikisha wanasimamia kwa karibu fedha zinazotolewa na serikali katika kutekeleza miradi mbalimbali ili ikamilike kwa wakati.

“Moja ya changamoto kubwa ni miradi kutokamilika kwa wakati hali ambayo inachangia hata Wizara ya Fedha kusimamisha baadhi ya miradi ambayo inachelewa kukamilika kutokana na kuongezeka kwa gharama za utekelezaji,” alisema.

Amesema katika eneo hilo wakurugenzi wengi wameshindwa kutimiza wajibu wao, hali ambayo imesababisha wengi wao kusimamishwa, kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na wengine kuondolewa nyadhifa zao.

Pia Nyamhanga amesema bado baadhi ya wakurugenzi wanashindwa kufanya matumizi ya mfumo wa 'Force Account'.

Aliwakumbusha wakurugenzi kuwa  wanatakiwa kutumia mwongozo mpya uliotolewa na Tamisemi, unaoelekeza matumizi sahihi ya utaratibu huo.

“Hivi sasa katika utaratibu wa force account kumekuwapo na changamoto ya vifaa kununuliwa kwa bei ya juu, lakini upendeleo kwa hawa mafundi tunaowatumia,” alisema Mhandisi Nyamhanga.

Vilevile amewasisitiza wakurugenzi wote kuhakikisha kuwa wanakamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuondoa msongamano ulipo katika shule mbalimbali.

“Tuhakikishe kuwa tunakamilisha vyumba vya madarasa katika muda uliopangwa ili kuondoa changamoto ya msongamao kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika mwaka wa masomo 2020,” alisema.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wanachama wa TOA, Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Rehema Madenge, alisema watahakikisha wanaitumia jumuiya hiyo kupeleka maendeleo kwa wananchi.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.