• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakuu wa Idara/Vitengo Jiji wahamishia kikao 'site'

Imewekwa tarehe: July 5th, 2019

Timu ya Uongozi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma (CMT) imeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mkonze kwa lengo la kuimarisha afya za wananchi na kujipanga kuhakikisha mipaka  ya kituo hicho inawekewa alama.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa timu hiyo ya uongozi ya Halmashauri, Shaban Juma baada ya kutembelea na kukagua ujenzi unaoendelea wa kituo hicho kilichopo katika Kata ya Mkonze.

Juma alisema kuwa hali ya ujenzi huo inaenda vizuri kwa mujibu wa ratiba ya kazi iliyopo. Alisema kuwa matarajio ya timu hiyo ya uongozi ya Halmashauri kuwa ujenzi huo utakamilika ifikapo tarehe 16 Julai, 2019 kwa mujibu wa mpango kazi uliopo.

Juma alisema kuwa maeneo ya mipaka ya kituo hicho cha afya yabainishwe na kuwekewa alama ili kuepuka uvamizi na makazi holela katika eneo la kituo hicho. Utambuzi na uwekaji wa mipaka ya kituo hicho utasaidia kuondoa migogoro na wananchi hasa kituo hicho kitakapohitaji upanuzi.  

Maelekezo mengine yaliyotiliwa mkazo ni kuongeza kasi ya utaratibu wa manunuzi ya milango 50 ukamilike na kupachikwa ili kuruhusu taratibu nyingine za ujenzi wa ndani ziweze kuendelea. Vilevile, uongoz wa kituo hicho cha afya ulielekezwa kufanya usafi wa mazingira ili kuboresha mandhari ya kituo hicho.  

Awali Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dkt. Baraka Chaula alisema kuwa serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya upanuzi wa kituo cha afya Mkonze kwa maelekezo. Maelekezo hayo aliyataja kuwa ni ujenzi wa jengo la wazazi, jengo la upasuaji, jengo la maabara, jengo la kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi.

Timu ya Uongozi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilihamishia kikao chake cha “Morning prayer’ katika miradi ya Kituo cha Afya Mkonze, shule ya msingi ya mfano inayojengwa Ipagala na eneo itakapojengwa shule ya sekondari ya mfano Iyumbu, kwa lengo la kukagua maeneo ya ujenzi huo na kuwa na uelewa wa pamoja juu ya miradi hiyo mitatu.


Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mkonze Baraka Chaula akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya kazi ya ujenzi kituoni mbele ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma


Wakuu wa Idara na Vitengo walipotembelea kuona maendeleo ya upanuzi wa kituo cha Afya Mkonze.


Mwalimu Joseph Mabeyo Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi wa Jiji la Dodoma akitoa maelezo kuhusu mradi, changamoto na mafanikio yaliyofikiwa katika ujenzi wa Shule ya Msingi ya Mfano.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.