• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakuu wa Mikoa, Wilaya hamasisheni wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya Korona - Dkt. Gwajima

Imewekwa tarehe: July 14th, 2021

KATIKA kupambana na ugonjwa wa Corona Serikali imewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchini kuhakikisha wanahimiza maelekezo yaliyotolewa na wataalam wa afya ya kudhibiti maambukizi ya awamu ya tatu ya virusi vya Korona (COVID 19) katika maeneo yao.

Amewataka kuhakikisha wananchi wanavaa barakoa wanapokuwa kwenye mikusanyiko, kufanya mazoezi, kutumia vipukusi mikono, kuzingatia matumizi ya lishe bora na kuhakikisha kunakuwa na maji tiririka kwenye maeneo yote ya mikusanyiko.

Agizo hilo limetolewa leo jijini hapa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima alipofanya ziara yake ya kustukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

"Viongozi wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha mnaendelea kutoa elimu kwa wananchi wenu hasa kipindi hiki ambacho wagonjwa wa Covid 19 wameanza kujitokeza ili maambukizi yasiendelee kuenea kwa kasi elimu hiyo itolewe kwa kutumia redio za kijamii na mikutano ya hadhara;

Rais Samia tayari alisema wagonjwa wapo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kibaigwa hivyo wananchi wanatakiwa kulichukulia suala hili kwa ukubwa wake na kuanza kuchukua tahadhari wao wenyewe kwasababu kila mtu anawajibu wa kutunza afya yake,"

Waziri Dkt. Dorothy amesisitiza kuwa wananchi waendelee kutumia tiba asili kwani serikali haijazuia matumizi ya tiba asili kwani imeweza kuisaidia jamii kwenye kudhibiti maambukizi ya Korona katika wimbi la kwanza, la pili hata la tatu pia itasaidia.

"Tusianze kupeana wasiwasi lakini pia ukiona dalili hizo haraka wahi kituo cha afya hiyo ndio vita tunatakiwa kupigana nayo" amesema Gwajima.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma kuhakikisha magari yote ya kubeba abilia hayajazi na hatua kali zichukuliwe kwa madereva watakao kiuka agizo hilo kwa mujibu wa vifungu vya sheria.

"Wamiliki wa magari katika hili mtatuvumilia katika hili tunataka maeneo yote ya magari yanapoanzia safari ya kwenda mikoani na maeneo mengine ndani ya mkoa tuhakikishe watu wamekaa kwenye ‘siti’ atakayekiuka agizo na kusimamisha watu njiani atachukuliwa hatua za kisheria kwasababu hapo tunaokoa maisha ya mtu" amesema Mtaka.

Aidha, katika eneo lingine Mtaka amewataka wafanyabiashara wote katika masoko wahakikishe wanavaa barakoa na katika milango yote ya kuingilia sokoni kuhakikisha kunakuwa na sehemu za kunawia mikono kwa kutumia maji tiririka.

"Katika maeneo ya minadani muhakikishe mnavaa barakoa kwasababu tunaposema suala la uhai wa mtu siyo suala la Serikali anapokufa mtu haifi Serikali wala hospitali, kanisa wala msikiti sisi kama Serikali tunakua tumetimiza wajibu" amesema Mtaka.

Sambamba na hayo pia amewataka Wakuu wa Wilaya zote wahakikishe wanaandaa vipindi kwenye redio za jamii ambazo ni rahisi hata wananchi waishio vijjini wajue namna ya kujikinga na kutoa matangazo kwenye maeneo ya mikusanyiko kuwakumbusha wananchi kuendelea kuchukua tahadhali.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma Mjini, Meja Msataafu Johnick Risasi alisema Covid 19 itadhibitika endapo kila mtu atatekeleza wajibu wake katika eneo lake kwasababu ni gonjwa la mlipuko ambalo litadumu kwa muda mrefu.

"Naishauri Serikali kuendelea kuweka sheria mbalimbali zenye lengo la kudhibiti maambukizi yasienee kwa kasi zikiwemo sheria kwenye Vyombo vya usafiri kutojaza abilia, kuhamasisha wananchi kunawa mikono kila mara itasaidia kuvuka salama katika wimbi hili la tatu," ameeleza.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.