• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wakuu wa taasisi 183 waruka kitanzi cha JPM

Imewekwa tarehe: January 25th, 2020

VIONGOZI wa taasisi, mashirika na makampuni 183 kati ya 187 wamenusurika kufukuzwa kazi baada ya kutekeleza agizo la Rais John Pombe Magufuli kwa kufanikiwa kutoa gawio na michango kwa serikali kiasi cha shilingi bilioni 25.12.

Aidha, taasisi nne zimeshindwa kulipa gawio na michango kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo kutokuwa na uzalishaji, upya wa taasisi na kampuni nyingine kurejeshwa serikalini kutokana na mwekezaji kutokidhi vigezo vya mkataba wa ubinafsishaji.

Novemba 24, mwaka jana, Rais Magufuli alizitaka taasisi, mashirika na kampuni kuwasilisha gawio na michango ya huduma za jamii ndani ya siku 60 ambazo zilikamilika jana saa sita usiku.

Akizungumza jana katika hafla ya kupokea hundi za gawio na michango, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, alisema agizo la Rais limetekelezwa kwa asilimia 100 na amevunja rekodi kwa kuwa haijawahi kutokea katika historia ya nchi.

"Kwa kweli zoezi hili kwangu halikuwa rahisi sana, nikifikiria uwingi wa idadi ya taasisi, mashirika na kampuni 187 ambazo hazikuwa zimechangia, nilijua kabisa lazima damu ya wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu itanimwagikia, lakini naona hali imekuwa tofauti kabisa," alisema.

Alisema mwenyekiti wa bodi yeyote na mtendaji mkuu husika angekuwa ameonyesha utovu wa nidhamu kwa kukaidi amri ya Rais alikuwa tayari kuwafukuza kazi jana na wangeondoka na aibu kubwa ya kushindwa mbele ya macho ya Watanzania.

"Kila siku huwa naeleza kuwa hii kazi ya Waziri wa Fedha ni ngumu, maana fedha nyingi zinahitajika, na kila sekta ili kutekeleza shughuli mbalimbali za serikali za kupeleka maendeleo kwa wananchi," alisema.

Alisema kuongeza ukusanyaji wa mapato na kulipa gawio na michango ya huduma za jamii kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali ni njia ya uhakika ya kujitegemea na kuondokana na fedheha ya kutegemea kuomba misaada nje ya nchi.

"Natamani awamu hii ikiisha tuwe tumefikia kukusanya Sh. trilioni mbili kwa mwezi, mwaka 2020 msisubiri Rais atoe maelekezo ndipo muanze kulipa gawio na michango," alisema.

Aliwataka viongozi wa taasisi hizo kuwajibika ipasavyo kuinua utendaji na kulipa gawio ili kuisaidia serikali kutekeleza shughuli za maendeleo.

Alisisitiza kupunguza matumizi yasiyo ya lazima katika mashirika na taasisi kwa kuwa si vyema nchi maskini viongozi wa taasisi kutanua.

Naye Msajili wa Hazina, Dk. Athuman Mbuttuka, alisema Rais alipokea gawio na michango kutoka kwa taasisi, mashirika na kampuni 79 kati ya 266 kiasi cha Sh. trilioni 1.05.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.