• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Walimu kata ya Ipagala wapongezwa kwa ufaulu wa wanafunzi

Imewekwa tarehe: June 29th, 2022

WALIMU wa Shule za Msingi na Sekondari zilizopo kata ya Ipagala Jijini Dodoma wamepongezwa kwa ufaulu wa wanafunzi wao katika mitihani ya Taifa kwa mwaka 2021/22.

Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. Omar Juma Kipanga wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo kwa walimu na wanafunzi wa kata Ipagala kufuatia hafla fupi iliyoandaliwa na Diwani wa Kata ya Ipagala Mh. Gombo Kamuli Dotto kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh. Anthony Mtaka na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mh. Anthony Mavunde.

“Niwapongeze sana walimu kwa kazi nzuri mnayoifanya, haya ni matokeo mazuri ya ushirikiano mzuri kati ya walimu, viongozi na wazazi.

Tunamshukuru Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma ambacho pia kinawagusa na ninyi walimu ikiwa ni sehemu ya kuthamini mchango wenu mkubwa katika maendeleo ya elimu.” Alisema Kipanga.

Akitoa maelezo ya awali Diwani wa Kata ya Ipagala, Mh. Gombo Kamuli Dotto amesema imekuwa ni utaratibu kwa kata hiyo kuwapongeza na kutoa tuzo kwa walimu na wanafunzi pindi wanapofanya vizuri na kuongeza morali ya kufanya vizuri zaidi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh. Anthony Mtaka ameitaka jamii kuthamini kazi nzuri inayofanywa na walimu na kuunga mkono jitihada za mkoa wa Dodoma katika kuinua viwango vya elimu kwa kuifanya Dodoma kinara wa elimu siku chache zijazo.

Mbunge wa Dodoma Mjini, Mh. Anthony Mavunde na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini kwa pamoja wamepongeza hatua hii ya kuenzi mchango mkubwa wa walimu na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kuendeleza sekta ya elimu Jijini Dodoma.

Pamoja na vyeti vya shukrani walivyopewa, walimu hao pia watapata fursa ya kutembelea Ngorongoro crater ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kukuza sekta ya Utalii nchini.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. Omar Juma Kipanga wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo kwa walimu na wanafunzi wa kata Ipagala Jijini Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.