• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Walimu wajivunia mafanikio miaka 28 ya chama, imo kuanzisha benki

Imewekwa tarehe: November 2nd, 2021

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) kimeadhimisha  miaka 28 tangu kianzishwe huku  kimeweka wazi mafanikio ambayo imeyapata ndani ya miaka hiyo ni pamoja na  kujenga majengo ya ofisi katika ngazi za Taifa, Mkoa na Wilaya, kuwa na uhusiano mzuri na wanachama wake, kuanzisha Benki ya mwalimu (MCBL).

Hayo yameelezwa leo November 1,2021 Jijini Dodoma na  Kaimu Rais wa Chama hicho,Dinnah Mathamani wakati  akizungumza na Waandishi wa Habari katika maadhimisho hayo

“Kweli tuna mafanikio makubwa kwa miaka 28 tumepambana tumefanikiwa mpaka hapa tulipo kwa mambo ambayo tumeelezwa pamoja na mafanikio mengi.

Hata hivyo ameelezea  changamoto walizionazo huku akiieleza Serikali kuwa waajiri wetu katika halmashauri zetu waliopo katika Halmashauri zetu na taasisi zingine zinazomshughulikia mwalimu.

“Kwanza nikieleza suala la stahiki za mwalimu bado mwalimu anamadai mbalimbali yasiyo ya mshahara na za mshahara nikieleza suala la uhamisho sisi kama chama cha walimu hatukatai wakati mwingine uhamisho unatokea ili kuweza kuleta tija na ufanisi sehemu za kazi.

“Lakini Serikali iliishasema unapomwamisha mtumishi hakikisha na maslahi yake tayari umeweka sawa lakini tumeeona waajiri wetu wanasema kurekebisha ikama lakini Je umeishamwandalia haki zake ? tumewasiliana na Wilaya mbalimbali walimu bado wana dai na walimu waliopo hapa ni mashuhuda

“Sasa tunaiomba Serikali lakini kwa ajili hasa katika halmashauri tuhakikishe tunaweka bajeti kwa ajili ya uhamisho zinazostahili si vyema kumwangaisha mwalimu anatoka sehemu moja kumpandisha maroli halafu unategemea akafanye kazi akiwa ametulia.

“Apate fedha zake za uhamisho ndio ahame Serikali wakati mwingine inatoa maelekezo mazuri lakini utekelezaji ndio unaleta shida leo tunawaambia kuna Halmashauri zinafanya vizuri kuna halmashauri zinafanya vibaya siku tutaleta mbele ya viongozi lakini pia ndani ya Serikali kwamba watu mliowapeleka kule hawawajibiki ipasavyo,”amesema.

Pia amesema changamoto nyingine ni suala la malipo ya  likizo pamoja na upandishwaji wa vheo kwa walimu.

Kwa upande wake,Katibu Mkuu wa CWT,Deus Seif amesema chama hicho ni moja kati ya vyama imara vya wafanyakazi ambapo wanajivunia kutetea na kusimamia vyema maslahi ya wanachama wake.

“Tumechagua kukaa meza moja na Serikali badala ya kuandamana na kwa hakika tumefanikiwa zaidi katika majadiliano kuliko katika maandamano.CWT tuna uhusiano mzuri na Serikali.Tunaishukuru Serikali kwa kutupa nafasi ya kukaa mezani  na kujadiliana,”amesema.

Naye,Mwekahazina wa Chama hicho,Abubakari Allawi amesema  katika miaka 28 ya uhai wa CWT imejenga na inaendelea kujenga majengo kwa ajili ya matumizi ya ofisi katika ngazi za Taifa,Mkoa na Wilaya.

Bw.Allawi  amesema mpaka sasa wana majengo 20 yanayotumika katika ofisi za chama  za Mikoa ambapo amedai majengo mengine matano katika Mikoa ya Simiyu,Geita,Njombe,Katavi, na Songwe yapo katika hatua za mwisho za ujenzi.

Anasema CWT inajenga majengo 38 ya ofisi katika ngazi za Wilaya ambayo yamegharimu zaidi ya shilingi milioni 315.

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu  majengo ya Mikoa 19 ya Wilaya yamefanyiwa ukarabati wa shilingi milioni 250 ambapo amedai tangu Ofisi za CWT zilipohamia Dodoma shughuli za Kitaifa zimekuwa zikifanyika katika jengo la Mkoa.

“Chama kimepanga kuanza ujenzi wa jengo la Makao Makuu mwaka 2022 na tutaendelea kukamilisha majengo matano ya Mikoa na 38 ya Wilaya ambayo yapo katika hatua za mwisho za ujenzi,”amesema.

Amesema kwa kipindi kinachoanza mwaka 2022 majengo mengine ya Wilaya yataanza kujengwa kwa kutumia mfumo wa Force Akaunti ili kupunguza gharama za ujenzi ukilinganisha na utaratibu wa kutumia mkandarasi,”amesema.

Amesema jengo pekee la CWT linalotumika kama kitega uchumi ni mwalimu House lilopo Ilala Jijini Dar es salaam ingawa kwa sasa makusanyo yake ya kodi yamepungua kwa asilimia 50 kutokana na shughuli za Kiserikali kuhamia Dodoma.

Kwa msaada wa Full Shangwe Blog



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.