• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waliohamia Dodoma wafurahia viwanja

Imewekwa tarehe: May 2nd, 2019

RISALA iliyosomwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa wa Dodoma wakati wa maadhimisho ya Sherehe za Mei Mosi Mwaka huu imeeleza jinsi wafanyakazi wa Wizara na Taasisi mbalimbali zilizohamia Makao Makuu ya Nchi Dodoma kutoka Dar es Salaam walivyofurahishwa na upatikanaji wa viwanja vya Makazi vilivyopimwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Risala hiyo ilisomwa wakati wa sherehe hizo zilizofanyika uwanja wa Jamhuri Jijini hapa mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge, ambapo viongozi mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa Wabunge na Mawaziri pia walihudhuria.

Aidha, pamoja na kuelezea furaha yao, wafanyakazi kupitia Shirikisho lao wameomba kuongezewa muda wa kulipia viwanja walivyonunua kufikia miaka mitatu badala ya miezi mitatu kutokana na hali ya kiuchumi kwa Wafanyakazi wengi kuwa ya kawaida.

Akizungumza na umati wa Wafanyakazi wa Serikali, Sekta Binafsi na wakazi wa Jiji la Dodoma waliofurika katika uwanja Jamhuri, Dkt. Mahenge aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupima viwanja vya matumizi mbalimbali kwa kasi inayoendana na mahitaji ya Dodoma ya sasa ambayo ni Makao Makuu ya Nchi.  

Akijibu ombi hilo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Mahenge aliahidi kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi kuweka utaratibu kwa makundi mbalimbali na watu binafsi kupewa muda wa kutosha wa kulipia kiwanja kulingana hali ya kiuchumi ya Wafanyakazi hao.

“Hata hivyo kuna baadhi ya maeneo ambayo ni lazima yaendelezwe haraka iwezekanavyo kutokana na mahitaji ya ukuaji wa Jiji kwa sasa, hivyo hili suala hatuwezi kulifanya kuwa la jumla” alifafanua Dkt. Mahenge.

Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani kwa Mwaka huu yaliongozwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania ya uchumi wa kati inawezekana, wakati wa mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi ni sasa”.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.