• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanahabari wapigwa msasa Wiki ya Unyonyeshaji

Imewekwa tarehe: August 4th, 2020

WIZARA ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Taasisi yake ya Chakula na Lishe imewapatia waandishi wa habari semina yenye lengo la kuwapa ufahamu kuhusu masuala ya lishe ya watoto wachanga na wadogo.

Semina hiyo imefanyika leo jijini Dodoma ikiwa ni mahususi katika Wiki hii ya Unyonyeshaji wa Maziwa ya Mama duniani ambapo Tanzania kama zilivyo nchi zingine inaadhimisha wiki hiyo ambayo hufanyika kila Agosti 1-7 ya kila mwaka.

Akizungumza katika semina hiyo Mkurugenzi Msaidizi kitengo cha Huduma za Lishe wa wizara ya Afya, Grace Moshi amesema maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji  hukumbusha umuhimu wa kuboresha hali ya lishe ya watoto kwa kufuata taratibu sahihi za unyonyeshaji maziwa ya mama pamoja na ulishaji wa watoto ili kujenga  msingi imara wa Afya na uhai wa watoto ambao ni Taifa la kesho.

Kwa upande wake Afisa Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya chakula na Lishe Tanzania, Neema Joshua amesema unyonyeshaji watoto maziwa ya mama hupunguza kiwango cha matumizi ya maziwa na vyakula mbadala vya watoto wachanga na wadogo.

Moshi Amesema lengo la kufanya semina hiyo kwa waandishi wa Habari ni kuwajengea uwezo na kuwahamasisha kuhusu suala zima la unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama na kuifikisha elimu hiyo katika jamii kupitia vyombo vya Habari.

Chimbuko la Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani ni azimio la Innocent la mwaka 1991 ambalo lilikuwa na  lengo la kulinda, kuhimiza na kuendeleza unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama ili kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake kuweza kunyonyesha watoto wao maziwa ya mama pekee katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo baada ya kujifungua na kuendelea kunyonyesha watoto wao hadi watakapotimiza umri wa miaka miwili au zaidi.

Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji yanakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘’Tuwawezeshe wanawake kunyonyesha watoto kwa Afya Bora na ulinzi wa Mazingira’’.

Hapa nchini wiki hii ilizindiliwa rasmi kitaifa Mkoani Tanga katika Halmshauri ya Muheza kwenye Uwanja wa Jitegemee  Agost 1,2020 na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

Mkurugenzi msaidizi Kitengo cha Huduma na Lishe Wizara ya Afya, Grace Mosha akitoa mada mbele ya wana Habari (hawapo pichani).


Neema Joshua, Afisa Mtafiti Mwandamini kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe alipokuwa akitoa mada kwa wanaHabari kuhusu Wiki ya Unyonyeshaji jiijini Dodoma.


Wanahabari wakishiriki kwenye mafunzo kuhusu Wiki ya Unyonyeshaji iliyofanyika jijini Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.