• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi 130,000 wa shule za msingi kupatiwa Kingatiba ya Minyoo na Kichocho Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: November 22nd, 2022

WANAFUNZI takribani 130,000 wa shule za msingi ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma wenye umri kuanzia miaka mitano hadi 14 kupewa kingatiba kwaajili ya kuzuia ugonjwa wa Kichocho na kutibu Minyoo.

Hayo aliyasema Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokutana na wataalamu wa afya kwenye ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwaajili ya semina ya utoaji kingatiba kwa wanafunzi wa shule za msingi.

Dkt. Method alisema kuwa zoezi hilo ni la muhimu sana kwasababu linakwenda kuzuia magonjwa ambayo yamekua yakiathiri watoto kwa wingi kutokana na mazingira wanayoishi wengi wao wanapata matatizo ya minyoo ambayo yanapelekea kupata tatizo la upungufu wa damu.

“Tukiangalia katika kundi hili unakuta anatembea bila kuvaa viatu au amekula kitu hajanawa mikono hali inayopelekea kupata minyoo, tunaenda kutoa kingatiba ili kuhakikisha tunawalinda dhidi ya maambukizi maana wanapopata maambukizi wanashindwa kuhudhuria masomo yao hivyo, kupelekea kushuka kwa viwango vya elimu. Kwakupewa kingatiba tunawahakikishia ulinzi ili wasije kukosa shuleni kwa sababu ya kupata ugonjwa wa Minyoo au kupata ugonjwa wa Kichocho,” alisema Dkt. Method.

Dkt. Method alisema Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaenda kutoa kingatiba za aina mbili ambazo ni Albendazo kwaajili ya Minyoo na Praziquantel kwaajili ya ugonjwa wa Kichocho. Dawa za Kichocho  zitatolewa kwenye kata nane ambazo ni Chigongwe, Chihanga, Ipala, Makutopora, Mbalawala, Mpunguzi, Nala na Mnadani. Alisema kuwa kata hizo zimeripotiwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Kichocho.

“Kimsingi tunaenda katika kipindi cha mvua kunasehemu ambazo zina madimbwi  ambayo ni maeneo rahisi kwa watoto kupata Kichocho, tunaenda kuwapa wanafunzi Kingatiba ili kuwalinda dhidi ya Kichocho. Nawashauri wazazi  washirikiane na walimu kuhakikisha wanafunzi wanakula chakula katika kata zote zitakazopewa dawa ya Kichocho ili kuepusha wanafunzi wasije kuanguka kwasababu ya njaa,’’ alisema Dkt. Method.

Akiongelea namna walivyojipanga Mganga Mkuu huyo alisema kuwa Jiji la Dodoma limejipanga kuhakikisha wanafunzi wote wanafikiwa na kupewa kingatiba. Zoezi litafanyika kwa siku moja tarehe 24 na kutakuwa na siku ya ziada  ya tarehe 25 kwaajili ya wanafunzi ambao walikosa shule  kwa sababu mbalimbali, aliongeza.

“Tunawataalamu wa afya ambao wamepewa mafunzo pia tumetoa mafunzo kwa walimu katika  shule za msingi ambao watashirikiana na wataalamu wa afya kuhakikisha kingatiba zinafika shuleni na wanafunzi wanapewa kwa usahihi. Wanafunzi watapewa kingatiba chini ya uangalizi wa walimu na wataalamu wa afya ili kuhakikisha wamekunywa kingatiba na wameweza kujilinda,’’ alielezea Dkt. Method.

Aidha, alitoa wito kwa  wazazi kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za msingi wanafika shuleni siku ya tarehe 24 Novemba ili waweze kupata kingatiba akiwahakikishia kuwa  hazina madhara yoyote ni salama kwa watoto.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.