• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi someni kwa bidii - Diwani Mkhandi

Imewekwa tarehe: January 25th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MWENYEKITI wa timu ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daud Mkhandi amewataka wanafunzi wa shule za sekondari kusoma kwa bidii ili waweze kufaulu na kuchaguliwa katika shule za kitaifa.

Agizo hilo alilitoa alipoongoza timu ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni na madarasa katika shule ya sekondari ya wasichana Bunge iliyopo jijini hapa.

Mkhandi alisema “tuwahamasishe wanafunzi kusoma sana na kufaulu ili waweze kuchanguliwa katika shule za sekondari za juu za kitaifa na kuweza kutoa mchango wao katika maendeleo ya taifa”.  

Kwa upande wa Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alisema kuwa jamii inatakiwa kuwasisitiza wanafunzi kusoma na kufaulu vizuri. “Mheshimiwa mwenyekiti, sisi halmashauri tutaendelea kusisitiza ufaulu mzuri kwa wanafunzi hasa kwenye shule za kata ili waweze kupangiwa shule za kitaifa kama hapa shule ya sekondari ya wasichana Bunge. Hakuna kigezo kingine zaidi ya viwango vya juu vya ufaulu” alisisitiza Myalla.

Awali Diwani wa Kata ya Kikombo, Emmanuel Manyono alisema kuwa shule ya sekondari ya wasichana Bunge kwa kuwa ipo Kata ya Kikombo, walitamani kuona watoto wa Kikombo wakipata fursa ya kusoma katika shule hiyo. “Tunatamani watoto wa Kikombo nao wanaofanya vizuri wawe wanachukuliwa hapa ili wananchi wetu wajivunie na kudumisha uhusiano mzuri na shule hii” alisema Manyono.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa madarasa mawili, mabweni mawili na viti na meza 60 kwa fedha za kuboresha shule za sekondari (SEQUIP), Mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Bunge, Salome Mkombola alisema kuwa shule yake ilipokea shilingi 244,200,000. “Mgawanyo wake ulikuwa shilingi 200,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili, shilingi 40,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na shilingi 4,200,000 kwa ajili ya viti na meza 60” alisema Mkombola.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.