• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi wa Ula sekondari watakiwa kudumisha nidhamu

Imewekwa tarehe: February 2nd, 2023

Na. Sekela Mwasubila, KONDOA MJI

WANAFUNZI wa kidato cha kwanza Katika Shule ya Sekondari Ula Halmashauri ya Mji Kondoa wametakiwa kuwa na nidhamu na kuzingatia sheria za shule walizopewa ili kuwa wanafunzi bora na kufanya vizuri katika masomo yao.

Hayo yamesemwa na Afisa Elimu Sekondari, Mwalimu Annette Nara alipokuwa akiongea na wanafunzi wa kidato cha kwanza waliopo katika shule hiyo wakati wa ziara ya ufuatiliaji aliyoifanya shuleni hapo.

“Kufaulu wote inawezekana ila ni jitihada zako mwenyewe kikubwa unapaswa kutunza nidhamu yako na kuepuka kujiingiza kwenye makundi ya utoro, ulaji wa mirungi na uvutaji wa bangi hawatakusaidia zaidi utapotea na ndoto zako,”amesema Mwalimu Nara.

Aidha, ameongeza kwa kuwaeleza kuwa wakumbuke wakifanya makosa ya utovu wa nidhamu mitaani watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za shule ambazo wanatakiwa kuzishika vizuri ili wapate matokeo mazuri na hawakufaulu kwa bahati mbaya.

“Mungu kakujalia ukafaulu hivyo soma kwa bidii kwa kuwa mwakani wana mtihani mna mtihani mwingine wa taifa wa kidato cha pili na maswali yote ya kiingereza ndio maana tunasisitiza pia kiingereza kitumike shuleni,”amesisitiza Mwalimu Nara

Aidha, amewasisitiza kutengeneza tabia ya kuongea kiingereza muda wote wanapokuwa shuleni si wanapomuona mwalimu tu kwani kwa kufanya hivyo hawataweza kujifunza na kuwataka kutoogopa kuchekwa kwa kuwa wanajifunza .

Amewaambia wanafunzi hao kuwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameleta fedha kwa ajili ya kuwa tengenezea mradi wa maji, kujenga madarasa mazuri na walimu wa kutosha hivyo ni jukumu lao kuhakikisha wanasoma kwa bidii na kupata daraja la kwanza na la pili.

“Na nyie watoto wa kike ni marufuku kuvua sketi zenu kwa vijana huko mitaani na tukikujua umevua utalala gerezani kwa kuwa unakuwa umetutia aibu wanawake wote mlindane wenyewe kwa wenyewe mkiona mwenzenu anakuwa na tabia mbaya toeni taarifa kwa Mkuu wa Shule na nyie wanaume mtusaidie kuwalinda dada zenu kwa kuwa hapa kazi ni moja tu ya kusoma,”amesema Mwalimu Nara.

Mwisho Mwalimu amewapongeza walimu wa shule hiyo kwa bidii wanayoionyesha ambapo kwa matokeo ya mwaka huu wamepunguza idadi ya wanafunzi waliopata sifuri katika matokeo ya kidato cha nne ambapo mwaka 2021 wanafunzi 27 walipata sifuri na mwaka 2022 wanafunzi 14 pekee wamepata daraja 0 na kuwataka kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayepata sifuri kwa mwaka 2023.

Shule ya Sekondari Ula ipo katika kata ya Kondoa Mjini kwa mwaka 2023 imepangiwa wanafunzi 309 na hadi kufikia Februari mosi wanafunzi 234 wameripoti na wanafunzi 25 wamehama na jitihada za kuwatafuta waliobakia zinaendelea.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.