• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi watakiwa kuacha usiri pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia

Imewekwa tarehe: June 5th, 2023

Na. Theresia Nkwanga, TAMBUKARELI

WANAFUNZI Shule ya Msingi Tambukareli watakiwa kuacha usiri na kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kutokomeza matendo ya ukatili wa kinjisia.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Viti Maalum wa Jiji la Dodoma, Joyce George alipokuwa akiongea na wananchi wa Kata ya Tambukareli pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Tambukareli iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

George alisema kuwa serikali inafanya jitihada  mbalimbali za kutokomeza ukatili wa kijinsia. Hivyo, wanafunzi hawapaswi kuogopa vitisho vya watu waliowafanyia ukatili wa kijinsia sababu serikali ipo nyuma yao kuhakikisha wanaoripoti taarifa za ukatili wa kijinsia wanalindwa.

“Kama unaogopa ukimripoti aliyekufanyia vitendo vya ukatili atakutukana na kukupiga niwaombe watoto wangu wazuri msiogope, msikubali kuzibwa midomo yenu kwa vitisho vyao huku mkiendelea kuvumilia maumivu makali ya ukatili wa kijinsia. Serikali ipo kwa ajili yenu imeweka vyombo vya sheria kuwasaidia katoeni ripoti kwa walimu wenu, wazazi, Polisi na kwa mtu yeyote wa karibu mnayemuamini. Msikubali kutishwa wala kuogopeshwa na mtu yeyote” alisema George.

Akielezea sababu za ukatili wa kijinsia kuendelea katika jamii, alisema kuwa Ukatili wa kijinsia kwa sehemu kubwa unafanywa na watu walio karibu. Hivyo, ili kumlinda ndugu huyo wa karibu, wahanga hawatoi taarifa ya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa na kusababisha vitendo hivi vya ukatili kuendelea katika jamii zetu.

“Niwaombe ndugu zangu tuache kuwakumbatia wahalifu wa ukatili wa kijinsia hata kama ni ndugu zetu, hili janga haliwezi kuisha kama tutachagua kufumba macho na kukaa kimya. Toeni taarifa kwa vyombo vya dola, Serikali na hata asasi za kiraia pindi unapofanyiwa au kushuhudia vitendo vya Ukatili wa Kijinsia kwa msaada zaidi wa kisheria. Tukishirikiana kwa pamoja na kuvunja ukimya tunaweza kulitokomeza janga hili la ukatili wa kijinsia na kulikomboa Taifa letu” alisema George

Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalum Jiji la Dodoma, Leticia Sanga Aliwashauri wanafunzi wa Shule ya Msingi Tambukareli wawe watoto wazuri wenye nidhamu, wawatii na kuwaheshimu wazazi wao. Pia wayashike na kuyatendea kazi mawaidha waliyopewa kuhusu ukatili wa kijinsia ili kuisaidia serikali katika mapigano dhidi ya kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.