• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi watakiwa kujengeana uwezo wa kujiamini

Imewekwa tarehe: February 28th, 2023

WANAFUNZI wa shule ya sekondari ya Viwandani iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujengeana uwezo katika kujiamini na kusaidiana ili waweze kufaulu katika masomo yao ya kuwa raia wema pindi wamalizapo shule.

Rai hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Viwandani katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tunu Dachi alipofanya ziara ya kutembelea shule hiyo na kuongea na wanafunzi hao jana.

Dachi alisema “tumekuja kwenu kuwaletea elimu ya vitu vikubwa vitatu. Kwanza ni suala la lishe bora, pili elimu ya kujitambua na tatu elimu kuhusu ukatili wa kijinsia. Nafahamu shuleni hapa kuna wanafunzi ambao mnaonea wenzenu. Wanafunzi kuoneana ni tabia mbaya. Tabia hiyo ndiyo mwanzo wa ukatili wa kijinsia. Wanafunzi mnapofanyiwa uonevu huo toeni taarifa kwa mwalimu wa zamu au mwalimu wa darasa. Lazima mjijengee uwezo na tabia ya kujiamini siyo kuoneana wala kudharauriana”.

Aliwataka wanafunzi hao kusaidiana katika masomo ili waweze kufaulu katika masomo yao. “Nilipokuja mara ya mwisho hapa kuongea nanyi nilisisitiza upendo na kusaidiana. Wanafunzi wenye uwezo katika masomo kama hisabati jengeni tabia ya kuwasaidia wenzenu ambao wana uwezo mdogo katika hisabati, fanyeni hivyo hivyo na kwa masomo mengine. Wadogo zangu nawahakikishia kufanya hivyo wote mtafaulu katika masomo yenu na mwisho wa siku mtakuwa kuwa raia wema kwa Halmashauri yetu. Na huu ndiyo mwanzo wa uzalendo kwa nchi yenu” alisema Dachi.

Akitoa elimu ya umuhimu wa lishe bora kwa wanafunzi, Afisa Lishe katika Mradi wa Lishe Endelevu, Aloyce Peter kuwa lishe bora ni muhimu kwa ukuaji wa vijana.  “Tunaposema kipindi cha ukuaji wa vijana ni miaka kati ya 10-19 kwa wavulana na wasichana. Hivyo, lishe bora ni vyakula ambavyo vinapatikana katika makundi matano ya vyakula na mchanganyiko wake ndio tunapata lishe bora au mlo kamili” alisema Peter.

Akiyataja makundi hayo ya vyakula na kazi zake alisema kuwa kundi la kwanza ni vyakula aina ya nafaka, mizizi pamoja na ndizi. Kazi yake ni kuupa mwili nguvu na nishati. “Kundi la pili ni vyakula asili ya wanyama na jamii ya mikunde. Kazi yake mwilini ni kuongeza madini chuma hasa kuwanufaisha watoto wa kike kuwasaidia kuongeza damu mwilini. Kwa vijana vinawasaidia kupata misuli na mwili mkubwa wenye nguvu. Kundi la tatu ni matunda. Matunda ya asili na ya kawaida tunayonunua sokoni. Matunda kazi yake ni kuimarisha kinga ya mwili na ufyonzaji wa vyakula tunavyokula” alisema Peter.

Akiongelea makundi mengine aliyataja kuwa ni vyakula vya mbogamboga ambavyo vinasaidia katika mmeng’enyo wa chakula na kuupa mwili madini mbalimbali. “Kundi la tano ni vyakula aina ya mafuta, sukari na asali. Vyakula hivi inashauriwa vitumike kwa kiasi kidogo kwa sababu vina nishati ya kutosha. Kama unakula mafuta mengi na sukari nyingi siyo mazuri mwilini. Sisi tupo katika kipindi cha ujana na katika kipindi hiki kuna ukuaji kupita kawaida, katika ukuaji huu lishe ni muhimu sana” alisema Peter.

 

MWISHO

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.