• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanafunzi wote ambao hawajaripoti shuleni watafutwe - RC Senyamule

Imewekwa tarehe: February 3rd, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameagiza wanafunzi wote ambao hawajaripoti shuleni watafutwe ili waweze kuripoti mapema na kuanza masomo akikemea vikali tabia ya wazazi kuwafundisha uvivu watoto wao.

Senyamule alitoa agizo hilo alipofanya kikao na kamati za maendeleo za kata nne ambazo wanafunzi waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Viwandani wanatoka, kikao kilichofanyika shuleni hapo.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa takwimu alizopata hadi jana zinaonesha kuwa shule ya sekondari Viwandani inaongoza kwa kuwa na kiwango kidogo cha wanafunzi kuripoti. “Wanaotakiwa kutafuta watoto hawa ni kamati za maendeleo za kata, wenyeviti wa mitaa na watendaji wa mitaa. Nilifahamishwa kuwa watoto wa shule ya sekondari Viwandani wanatoka katika kata nne ndiyo maana nikaitisha kikao na kamati za maendeleo za kata hizo ili tuweze kuulizana walipo watoto hao” alisema Senyamule.

Wakati huohuo, alipongeza ongezeko la watoto kuripoti ngazi ya mkoa hadi kufikia asilimia 78. “Niwapongeze kuwa watoto wameweza kuongezeka. Wiki iliyopita tulikuwa na asilimia 69 kimkoa ila mpaka jana tulikuwa na asilimia 78 kimkoa. Lakini bado asilimia 78 ni ndogo kuna kama asilimia 22 ambao hawajaripoti kwa kidato cha kwanza. Bado tunakazi kubwa ya kufanya. Tumieni mtandao wa watendaji ili wanafunzi watafutwe wote ambao hawajaripoti shule waweze kuripoti” alisema Senyamule.

Vilevile, alikemea tabia ya baadhi ya wazazi kuwafundisha Watoto wao uvivu. Alisema kuwa wapo baadhi ya wazazi ambao wanawaruhusu Watoto wao kuchelewa kuripoti shuleni kwa kisingizio kuwa masomo hayajaanza na hatimae kushindwa kwendana na kasi ya mwalimu.

Kwa upande wa Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Upendo Rweyemamu alisema kuwa changamoto moja wapo ni wazazi wanapohamisha wanafunzi kutoka shule ya sekondari viwandani hawatoi taarifa kwa uongozi wa shule huyo.

 “Mheshimiwa mgeni rasmi, utaona shule ya sekondari Viwandani ina asilimia ya chini kabisa ya kiwango cha kuripoti, ina asilimia 42. Shule hii inalishwa na shule nne za msingi, shule tatu ni za binafsi na moja ya serikali. Wazazi wanapoamua kuwapeleka wanafunzi shule binafsi hawarudi kutoa taarifa kwa shule husika” alisema Rweyemamu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.