• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi Kata ya Kikuyu Kaskazini wafurahia huduma ya kujifungua Zahanati ya Kikuyu

Imewekwa tarehe: April 17th, 2025

Na. Leah Mabalwe, KIKUYU KASKAZINI

KATA ya Kikuyu Kaskazini yajivunia maboresho ya huduma za afya kwa kina mama jambo linalopunguza uwezekano wa vifo vya kina mama wajawazito na wakati wa kujifungua katika Zahanati ya Kikuyu.

Akiongea na waandishi wa habari waliotembelea Zahanati ya Kikuyu kujionea utoaji wa huduma katika jengo la wazazi ikiwa ni ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali kwa kipindi cha miaka minne kwenye Kata ya Kikuyu Kaskazini.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Kikuyu, Dkt. Azania Silliah alimshukuru Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, kwa kuwapatia shilingi 33,612,800 kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa jengo la wazazi. Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma aliwapatia shilingi 50,000,000 kwaajili ya umaliziaji wa jengo hilo.

“Napenda kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzani kwa kuona umuhimu wa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Nipende kumshukuru Mbunge wetu, Anthony Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kwaajili ya kuhakikisha wazazi wanapata huduma nzuri wakati wa kujifungua kwa kutoa fedha ya uanzishaji wa mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kikuyu. Pia namshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kuunga mkono jitihada za mbunge wetu” alishukuru Dkt. Silliah.

Mwananchi Johari Issa alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kujenga jengo la wazazi katika Zahanati ya Kikuyu. “Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutujengea jengo la wazazi la kujifungulia pamoja na huduma ya mama na mtoto, kwasababu hapo awali tulikuwa hatuna kabisa jengo la wazazi. Tulikuwa tukitembea umbali mrefu kwaajili ya kufuata huduma ya kujifungua kutoka sehemu moja kwenda nyingine na tulikuwa tunapata shida kwasababu muda mwingine tunatembea usiku kwaajili ya kufuata huduma. Kwa hivi sasa hatupati tena adha ya kutembea umbali mrefu kwasababu huduma imesogezwa karibu” alishukuru Issa. 

Kwa upande wake, Imelda Kessa aliipongeza serikali kwa kuwapelekea vifaa vya kisasa kwaajili ya kujifungulia katika jengo la wazazi. “Naishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutuwekea vifaa vya kisasa, katika zahanati yetu ya Kikuyu. Hii zahanati ni ya mfano kwasababu kuna vifaa na huduma nzuri zinazotolewa hasa wazazi kujifungua. Zahanati ina wauguzi wabobezi katika kazi yao” alipongeza Kessa.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.