• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

wananchi Kata ya Msalato wamshukuru Rais Dkt. Samia kwa kuwajengea shule

Imewekwa tarehe: March 7th, 2024

Na. Dennis Gondwe, MSALATO

WANANCHI wa Kata ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamemshukuru Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mpya na kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu.

Shukrani hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara alipokuwa akiwatambulisha wataalam wa kata yake katika Shule ya Msingi Chikole kwa mgeni rasmi Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma.

Selufara alisema “Shule ya Msingi Chikole ina wanafunzi 790 ilianza mwaka jana mwezi Julai. Baada ya kumaliza ujenzi ulioanza mwezi Aprili, 2023 kwa fedha ya mama Samia Suluhu Hassan aliyotupatia shilingi 318,800,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Chikole, ambapo tulijenga madarasa tisa, matundu 16 ya vyoo, jengo la utawala moja, tumefanikiwa kujenga madarasa ya chekechea ya mfano ni kama shule za mchepuo wa kiingereza pamoja na madawati yanayotosheleza madarasa yote. Cha kufurahisha zaidi serikali yake imetujengea kisima cha maji chenye thamani ya shilingi 22,500,000, hivyo shule hii ni mahali salama kabisa kwa watoto wetu.

Kwa kuwa umefika hapa kiongozi wetu mkubwa wa kimkoa tunaomba utufikishie salamu sisi wananchi wa Kata ya Msalato za pongezi kwa kuweza kutukumbuka kutujengea shule hii na kuwapunguzia wanafunzi wetu kutembea mwendo mrefu”.

Aliongeza kuwa Rais, Dkt. Samia alitoa fedha shilingi 680,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa saba, mabweni manne na vyoo vyenye matundu 10 katika Shule ya Sekondari ya wasichana Msalato. “Mheshimiwa mgeni rasmi, mama huyu hakuishia hapo, alitupatia fedha shilingi 437,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Msalato pamoja na madawati yake. Ambapo tulijenga madarasa 12, matundu 12 ya vyoo, ofisi mbili za walimu pamoja na eneo la kunawia mikono” alisema Selufara.

Afisa mtendaji huyo aliongeza kuwa walianza kujenga kituo cha afya kwa nguvu za wananchi zenye thamani ya shilingi 50,000,000 hadi usawa wa lenta. “Serikali ya mama Samia imetupatia fedha shilingi 30,000,000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa kituo hicho cha afya. Tunamshukuru sana mama yetu. Vilevile, tumejenga zizi la ng’ombe kwa shilingi 19,800,000. Kwenye Kata hii ya Msalato. Rais mama Samia ametoa karibia shilingi bilioni 1.3 kwa mwaka wa fedha 2023/2024” alisema Selufara.

Akiongelea zawadi za unga wa mahindi, maji, kalamu, na taulo za kike kwa shule za Kata ya Msalato alisema ni michango ya wananchi wa Msalato. “Hii ni michango ambayo tumeshiriki pamoja wanaume na wanawake tumeona tuadhimishe na ninyi watoto wetu wa shule za msingi na sekondari. Tunawashukuru wote walioguswa afya njema” alisema Selufara.

Maadhimisho ya siku ya wanawake Kata ya Msalato yalifanyika kwa kutoa elimu ya lishe bora kwa wanawake na hamasa ya kujishughulisha yakifanyika katika Zahanati ya Msalato inayozungukwa na mitaa sita ikikadiriwa kuhudumia watu 11,000.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.