• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi Mtumba kulipwa fidia zao - Mkurugenzi Jiji

Imewekwa tarehe: August 16th, 2020

WANANCHI 34 wa kata ya Mtumba ambao hawakuwepo wakati wa uthamini watalipwa fidia za ardhi yao na Halmashauri ya Jiji la Dodoma mwishoni mwa mwezi huu wa nane 2020.

Hayo yalisemwa jana na mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alipokuwa akijibu swali la mwananchi wa Kata ya Mtumba, Jackson Seganje aliyetaka kujua malipo ya fidia kwa wananchi 34 ambao hawakuwepo katika uthamini uliopita wa eneo la Mtumba. Mafuru alisisitiza kuwa malipo hayo yatalipwa mwisho wa mwezi Agosti mwaka huu.

Mafuru ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Mipango miji, Ardhi na Maliasili katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, ni kweli kuna wananchi 34 ambao kwenye eneo tulilotwaa hawakuwepo wakati wa zoezi la uthamini. Eneo ambalo tulitwaa tulirudia mara nne zoezi la uthamini. Hii ni kwa sababu mnaweza kufanya zoezi hilo lakini bahati mbaya wachache wasiwepo wakati wa utekelezaji zoezi hilo, kuna kitu kinaitwa ‘supplementary valuation’ kwamba watakapokuwa wale watu tutawafanyia kitabu cha pili ili wa kwanza wanalipwa kwanza na wale wengine wanalipwa baadae. Sasa hawa waliobaki wananchi 34 ni wa awamu ya tano ambapo wanadai shilingi milioni 210” alisema Mafuru.

Mkuu huyo wa Idara alikiri kuwa wananchi hao walipaswa kulipwa mwaka wa fedha ulioisha ila taratibu hazikukamilika na kuahidi malipo hayo kufanyika kufikia mwisho wa mwezi Agosti, 2020. “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ninachoweza kukuahidi pamoja na wananchi hawa ni kwamba kabla ya mwezi huu Agosti kuisha fedha zao zitakuwa kwenye akaunti zao. Malipo haya ni kipaumbele kwetu kwa sababu tulifunga nayo mwaka wa fedha uliopita” alisema Mafuru kwa kujiamini.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini (wa pili kutoka kulia waliokaa) akimsikiliza kwa makini Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji Joseph Mafuru (aliyesimama mbele) wakati akijibu swali la mwananchi wa Mtumba (hawapo pichani) kuhusu fidia ya wananchi wa eneo hilo. Wengine pichani, kushoto ni David Msasa Afisa Tarafa wa Kikombo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo kata ya Mtumba Nathanael Mlunya (wa tatu kulia waliokaa mbele) na Dionis Samo (wa kwanza kulia mbele) ambaye ni Mtendaji wa Kata ya Mtumba.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.