• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi wa Dodoma watakiwa kukemea na kuondokana na tabia za ukatili wa kijinsia

Imewekwa tarehe: December 10th, 2024

Na. John Masanja, DODOMA

Wananchi wa Dodoma wametakiwa kukemea na kuondokana na tabia za ukatili wa kijinsia unaofanyika ndani ya jamii wanazoishi ili kuandaa jamii iliyobora na yenye maendeleo kwa taifa.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alipokuwa akizungumza na hadhira katika Kongamano la kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, lililofanyika katika ukumbi mikutano wa 'Dear Mama' jijini Dodoma.

Aidha, Senyamule alizitaja takwimu za mwenendo wa matukio ya ukatili mkoani Dodoma, alisema kuwa kwa Mwaka 2023 (Januari - Agosti) matukio yaliyoripotiwa yalikuwa 3,012 huku watoto wakiwa ni 846 na watu wazima ni 2,166. Pia alisema kwa Mwaka 2024 (Januari - Agosti) matukio yamepungua hadi kufikia 2,352 huku watoto wakiwa 529 na watu wazima wakiwa 1,723.

Sambamba na hilo, Senyamule alitoa rai kuwa jamii iendelee kuelimishwa kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia na kuwataka wananchi kutosita kutoa ushirikiano endapo kuna viashiria au ufanyikaji wa vitendo vya ukatili ili hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika.

"Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa akifanya jitihada kubwa katika kutokomeza ukatili wa kijinsia, amefanya mambo mengi baadhi yake ni ujenzi wa Shule zakutosha, utoaji wa mikopo kwa wanawake, urahisishaji wa huduma kama ya upatikanaji wa maji pamoja na uwepo wa nishati safi. Hayo yote ukiyatazama Kwa undani, yamechangia kwa sehemu kubwa kupunguza matatizo hayo ya ukatili wa kijinsia" alisema Senyamule.

Senyamule alisema yupo tayari kutoa msaada na ushirikiano kwa yeyote atakayetoa taarifa katika ofisi yake kuhusu utendekaji wa matukio ya kikatili ya kijinsia.

"kila mmoja akatimize wajibu wake kwa kuhakikisha hakuna tendo la kikatili linalotendeka mbele yake, kwa kufanya hivyo tutaikomboa Dodoma" alisema Senyamule.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP. George Katabazi, alisema Jeshi la polisi limeendelea kupambana dhidi ya matendo ya ukatili wa kijinsia na kwa kupitia siku 16 za kampeni ya kutokomeza ukatili wa kijisia, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limefanya shuguli kadha wa kadha ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kupitia dawati la jinsia na kufanya matendo ya huruma kwa wahitaji na waathirika wa matendo ya kikatili.

Vile vile, Kamanda Katabazi, alisema Jeshi la Polisi halitaacha kuchukua hatua kwa yeyote atakaefanya vitendo vya ukatili na hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

"Kwa pamoja niwaombe wananchi tushirikiane kutokomeza ukatili wa kijinsia ndani ya jamii zetu kwa ustawi na maendeleo ya taifa letu" alisema Kamanda Katabazi.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj. Jabir Shekimweri, aliwataka wananchi kuepukana na mila potofu zinazipelekea kutendeka kwa matendo ya ukatili ndani ya jamii na kuwataka wananchi kuwa na hofu ya Mungu ili kuepukana na vitendo hivyo.

Aidha, Shekimweri aliwataka wananchi kutumia muda wao katika siku hii ya kilele cha maadhimisho ya kupinga ukatili wa kijinsia, kujitafakari na kubaini sababu zingine zinazopelekea matendo hayo na alitoa rai kwao kuyaacha mara moja.

"Niwapongeze na kuwashukuru wadau mbalimbali wanaoisaidia Serikali katika kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia, kiukweli mnafanya kazi nzuri sana na msiache kufanya hivyo" alisema Shekimweri.

Akitamatisha salamu zake, Shekimweri alimshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada anazozifanya katika kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Sambamba na hilo alitoa kongole kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP George Katabazi, kwa namna nzuri ya uongozi wake unaoleta manufaa mkoani Dodoma.

Ikumbukwe kuwa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia hufanyika kuanzia tarehe 25 Novemba hadi tarehe 10 Desemba kila mwaka, kwa mwaka 2024 maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yameongozwa na kauli mbiu inayosema “Kuelekea Miaka 30 ya Beijing: CHAGUA Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.