• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi waiomba Serikali kupeleka huduma za kibingwa mahali walipo

Imewekwa tarehe: October 26th, 2021

Na Mwandishi Maalum – Dodoma

WANANCHI wa Mkoa wa Dodoma wameiomba Serikali kutoa huduma za matibabu ya kibingwa za kuwafuata wananchi mahali walipo mara kwa mara kwa kufanya hivyo wananchi wengi zaidi hasa walioko vijijini watafikiwa na huduma hizo.

Ombi hilo limetolewa leo jijini Dodoma na baadhi ya wananchi waliofika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival linalofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma.

Wananchi hao walisema kupatikana kwa huduma hizo katika tamasha hilo kumewafanya wapate nafasi ya kupima afya zao kwa gharama ndogo tofauti na ambavyo wangesafiri na kuzifuata jijini Dar es Salaam.

“Nimefika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) nimepokelewa vizuri nimepimwa uzito, urefu, kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi pamoja na umeme wa moyo, nimepewa dawa za kutumia pamoja na ushauri wa lishe bora kwa afya ya moyo”.

“Ninaiomba Serikali iendelee kutoa huduma kama hizi hasa maeneo yaliyo mbali na Dar es Salaam kwani siyo kila mwananchi anauwezo wa kwenda kupata huduma kama hizi Dar es salaam”, alisema bibi Theresia Duwe mkazi wa maili mbili jijini Dodoma.

“Tunazishukuru taasisi za afya kwa kutusogezea karibu huduma za matibabu ya kibingwa, mimi na wenzangu tumepata huduma za vipimo, ushauri na dawa. ninawaomba wananchi wenzangu watumie nafasi hii kuja katika viwanja hivi kupima na kutambua hali zao”, alishukuru mama Sada Kitenge mkazi wa area c jijini Dodoma.

Kwa upade wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Doroth Gwajima ambaye alitembelea banda la taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa JKCI alisema Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya zikiwemo za matiba ya kibingwa.

“Ukiangalia idadi ya watu waliojitokeza kupima pamoja na matatizo ya moyo waliyokutwa nayo kuna haja ya Serikali kutoa elimu ya kutosha ya jinsi ya kuepukana magojwa haya pamoja na kuhakikisha wale wanaokutwa na matatizo mara baada ya kufanyiwa upimaji wanapata dawa za kutumia”, alisema Dkt. Gwajima.

Huduma zinazotolewa katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ni upimaji wa urefu na uzito, kiwago cha sukari kwenye damu, shinikizo la damu (BP), kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography), kipimo cha mfumo wa umeme wa moyo (Electrocardiography), kutoa dawa kwa watu watakaokutwa na matatizo ya moyo na rufaa ya moja kwa moja ya kwenda kufanyiwa uchunguzi zaidi katika taasisi hiyo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akiangalia dawa za moyo zinazotolewa bila malipo na  kampuni ya uagizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Sun Pharmaceutical Industries Ltd. Kwa wagonjwa wanaokutwa na matatizo ya moyo waliofika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival linalofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma.

Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwahudumia wananchi  waliofika  katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival linalofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma.

Mwakilishi wa kampuni ya uagizaji na usambazaji wa dawa za binadamu ya Sun Pharmaceutical Industries Ltd. Bruno Mlowe akitoa maelekezo ya jinsi ya kutumia dawa za moyo kwa wananchi waliofika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival linalofanyika katika viwaja vya Chinangali park jijini Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.