• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi wakumbushwa kuzingatia kanuni za afya

Imewekwa tarehe: February 3rd, 2020

Afisa Afya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Abdallah Mahia amewataka  wananchi kuzingatia kanuni za afya kwa waandaji wa vyakula majumbani na hata wauzaji wa vyakula na vinywaji, kuzingatia matumizi ya vifaa kinga (sare za kazi - 'uniform')  ili kuweza kuzuia magonywa ya kuambukiza.

Mahia ameyasema hayo leo katika kituo cha Radio cha Dodoma FM kwenye kipindi cha 'Dodoma live' alipokuwa anaeleza kuhusiana na maambukizi ya sumu inayosababishwa na kuchafuka kwa chakula, maji au kinywaji kutokana na bakteria na vimelea mbalimbali jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha ya watu  na kusababisha madhara endapo mtu atakula chakula hicho.

Mahia alieleza vihatarishi vinavyoweza kusababisha maambukizi kwenye chakula, ambapo aliyataja baadhi ya maeneo ambayo ni hatarishi zaidi na yanahitaji umakini mkubwa katika uandaaji wa chakula.

“Maambukizi kwenye chakula hutokea zaidi katika vyakula vilivyoandaliwa katika misiba, kazini, matanga, hitma, ngoma, harusi na mikusanyiko inayohusisha ulaji wa chakula kwa pamoja ambapo mtu mmoja au kundi la watu  hupata ugonjwa kutokana na kutozingatia kanuni za afya.

“Watoto wadogo pamoja na wazee ni makundi ambayo yanaathiriwa zaidi kutokana na kinga zao kuwa chini, wanapopata bakteria mwili unashindwa kupambana navyo,  pamoja na watu wenye matatizo ya kiafya, magonjwa ya figo na kisukari, wenye upungufu wa kinga mwilini, na wasafiri wanaotembelea maeneo yanayojulikana kuwa na vimelea vinavyosababisha hali hii kwa wingi,” alisema Mahia.

Afisa afya huyo alifafanua juu ya dalili za mtu ambaye tayari ameathiriwa na sumu kwenye chakula pamoja na kuelekeza madhara yatokanayo na ugonjwa huo.

“Vimelea vya sumu huingia kwenye chakula wakati wa maandalizi na upikaji mbaya, utumiaji wa maji yasiyo salama yenye vimelea vya kinyesi, mikono pamoja na vyombo vikiwa vichafu, kachumbari isiyoandaliwa kwa usafi, matunda  yasiyooshwa na mboga za majani zisipoiva vizuri, nyama isipoiva vizuri, na mayai mabichi.

“Dalili za mtu mwenye maambukizi kwenye chakula ni maumivu ya tumbo, homa na kujihisi baridi, kuumwa kichwa, kichefuchefu na kutapika, kuharisha majimaji au damu, mwili kuwa dhaifu na ulegevu unaosababisha mtu kushindwa kupumua na hatimaye husababisha kifo.

“Madhara hutegemea na aina ya bakteria anayesababisha ugonjwa huu, lakini mengi huwa ni kupata matatizo ya figo, kutokwa na damu bila kukoma, magonjwa ya viungo ya mwili, magonjwa ya mfumo wa fahamu na madhara katika moyo,” aliongeza Afisa Afya.

Aidha, alisema visababishi vinavyosababishwa na maambukizi kwenye chakula ni pamoja na vimelea vya bacteria na virusi ambapo alisisitiza juu ya kuhakikisha kunawa kwa maji ya moto na sabuni mara baada ya kutoka chooni, na  baada ya kutoka, kumnawisha mtoto anapokuwa amejisaidia na kusisitiza suala la usafi kuzingatiwa jijini kote.

Pia amesisitiza wananchi hasa katika kipindi cha mvua kuhakikisha wanazingatia matumizi sahihi ya vyoo, kuepuka kujisaidia kwenye vyanzo vya maji na kuepuka kutiririsha au kufungulia vyoo kuelekea kwenye maji ya mvua. Mahia amesisitiza katika Jiji la Dodoma magonjwa ya kuambukizwa ni historia hivyo ametoa onyo kwa yeyote atayekaidi taratibu za afya, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.