• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanawake jiungeni CHF mboreshe afya, mkopesheke-Afisa Maendeleo

Imewekwa tarehe: July 10th, 2019

WANAWAKE katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali ili waweze kukopeshwa fedha kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alipokuwa akihamasisha  wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa katika uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji mkubwa wananchi iliyofanyika katika mtaa wa Mahomanyika uliopo kata ya Nzuguni jijini hapa.

Nabalang’anya alisema kuwa mfuko wa afya ya jamii ni muhimu zaidi kwa kina mama. “Kina mama tuwashawishi waume zetu sababu mara nyingi ndiyo washika fedha ili tujiunge na CHF na kuweza kupata huduma ya matibabu bure kwa watu 6 mwaka mzima kwa shilingi 30,000 tu” alisema Nabalang’anya. Mara zote ugonjwa haupigi hodi, hivyo wananchi wanatakiwa kujiandaa kukabiliana na ugonjwa kwa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa, aliongeza.

Kutokana na ukweli kuwa wanawake ndiyo wanaobeba jukumu kubwa katika familia, afisa maendeleo ya jamii huyo aliwashauri kujiunga katika vikundi. Alisema kuwa kujiunga katika vikundi kutawawezesha kupata mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa ajili ya kufanya shughuli za maendeleo. Kupitia shughuli hizo za maendeleo kina mama wataweza kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa kwa kuchangia shilingi 30,000 na watu sita kuhudumiwa matibabu mwaka mzima, aliongeza.

Nae Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma mjini, Edward Mpogolo alisema kuwa Rais wakati akinadi ilani ya uchaguzi aliahidi kuhakikisha wananchi wanajiunga na Mfuko wa Bima ya Afya ili wawe na afya bora. “Kujiunga na CHF ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Magufuli za kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na afya bora” alisema Mpogolo.

Awali mratibu wa CHF katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga alisema kuwa lengo la maboresho ya CHF ni kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanajiunga na mfuko huo ambao utawasaidia kupata huduma za afya kwa gharama nafuu.

Akiongelea hali ya wanachama, alisema kuwa idadi ya kaya zilizojiunga na mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa kuanzia Julai, 2018 hadi Juni, 2019 kwa kiwango cha shilingi 30,000 ni kaya 3,155. Idadi hiyo aliitaja kuwa ni sawa na asilimia 3.4 ya kaya zote zilizopo katika Halmashauri ya jiji la Dodoma.

Wananchi wa Mahomanyika wakimsikiliza Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji Sharifa Nabalang'anya (hayupo pichani) wakati wa kampeni 

ya kuhamasisha watu kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamaii ulioboreshwa.

Wakazi wa Mahomanyika wakimsikiliza Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji (hayupo pichani) akifafanua faida za kujiunga katika vikundi 

ili kupata mikopo na umuhimu wa kujiunga na CHF iliyoboreshwa.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.