• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanawake waaswa kufanya mazoezi kuimarisha afya

Imewekwa tarehe: March 6th, 2021

WANAWAKE jijini Dodoma wametakiwa kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika michezo mbalimbali ili kuimarisha miili na afya zao.

Kauli hiyo ilitolewa na kaimu Mkurugenzi, Idara ya Maendeleo ya Jamii, Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Mboni Mgaza alipoongoza mamia ya wakazi wa Jiji la Dodoma kushiriki katika tamasha la michezo likiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani.

Mgaza alisema kuwa michezo ni muhimu katika kuimarisha afya na inasaidia kuimarisha mwili na kuusaidia kuepukana na maradhi nyemelezi. “Ukiwa mwanamichezo maradhi hayatakuvamia kwa sababu mwili utakuwa imara. Hivyo, michezo inaimarisha mwili na kuifanya akili kuwa timamu na kufikiria haraka tofauti na asiyeshiriki michezo” alisema Mgaza. Michezo inajenga mahusiano mazuri katika jamii kwa mtu mmoja mmoja na baina ya taasisi na taasisi, aliongeza.

Kwa upande wa mratibu wa tamasha hilo, Elizabeth Kasimila alisema kuwa aliandaa tamasha la michezo katika maadhimisho kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani ili kuwapa wanawake nafasi ya kushiirki michezo na kuweka miili yao katika hali nzuri.

“Leo, tumefanya mazoezi ya kutosha ili siku ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani tuwe na afya bora kushiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani na kutembelea maeneo mbalimbali” alisema Kasimila.

Kasimila ambae pia ni Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Catalyst for Community Transformation Organization (CFCTO) alisema kuwa taasisi yake kwa kushirikiana na taasisi nyingine binafsi na serikali waliona jambo la mazoezi ni jema katika kujenga miili na afya ili kuepukana na maambukizi mbalimbali. “Kumekuwa na milipuko na maradhi tofauti, mtu akipata mafua kidogo anatetereka, hivyo tunaamini mazoezi ni tiba kwa mwanadamu” alisema mratibu huyo. Aidha, aliishukuru benki ya CRDB kwa kufadhili tamasha hilo.

Kwa upande wa mshiriki kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Elinajoyce Petro alisema kuwa michezo hiyo ni muhimu kwa afya. “Mazoezi haya ni muhimu kwa afya zetu kwa sababu yanatusaidia kujenga miili yetu, kujenga kinga ya mwili na magonjwa yasiyo ya kuambuliza yanazuiwa kwa kufanya mazoezi. Kwa wale ambao siyo watumishi wa umma wanakaribishwa kufanya mazoezi kila siku hapa uwanja wa Jamhuri kuanzia saaa 12 alfajiri” alisema Petro.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Wanawake katika uongozi, ni chachu kufikia dunia yenye usawa” na katika Jiji la Dodoma yatafanyika katika uwanja wa Nyerere Square.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.