• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wanawake wapanda miti 200

Imewekwa tarehe: March 7th, 2020

KAMATI ya Maandalizi ya siku ya wanawake Duniani Mkoa wa Dodoma imepanda miti 200 katika kituo cha Afya Mkonze na shule ya msingi Mkonze kwa lengo la kuihamasisha jamii kupanda miti kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kauli hiyo ilitolewa na mratibu wa kamati ya maandalizi ya siku ya wanawake duniani Mkoa wa Dodoma, Fatuma Daud alipokuwa akiongezea zoezi la upandaji miti lililofanywa na kamati hiyo kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani jana katika kata ya Mkonze.

Fatuma alisema kuwa kamati iliamua kwenda kupanda miti 100 katika eneo la shule ya msingi Mkonze na miti mingine 100 katika kituo cha Afya Mkonze. “Lengo la kupanda miti katika maeneo hayo ni kuihamasisha jamii kuona jukumu la kupanda miti ni la jamii nzima. Tumepanda miti 100 katika shule ya msingi Mkonze kwa lengo la kuifanya shule hiyo kuwa eneo salama kwa watoto kusoma, lakini pia kuwajengea wanafunzi wa shule hilo kuona wana wajibu wa kupanda na kutunza miti katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi” alisema Fatuma. Katika kituo cha Afya Mkonze, tuliona ni vizuri kuwa sehemu ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira ili kituo cha Afya hicho kiwe na mandhari na hali nzuri ya hewa ambayo kwa upande mwingine ni tiba kwa wagonjwa, aliongeza Fatuma.

Fatuma, ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa kamati ilichagua kwenda kupanda miti katika eneo hilo ukiwa ni mkakati wa kuwafanya wananchi wanaozunguka eneo hilo kuwa tayari kupokea tukio la kilele cha siku ya wanawake duniani. “Kilele cha siku ya wanawake duniani ngazi ya Mkoa wa Dodoma kitafanyika katika shule ya msingi Mkonze, hivyo zoezi la upandaji miti katika shule na kituo cha Afya ni kuwaandaa wananchi kupokea tukio hilo muhimu litakalofanyika Jumapili tarehe 8 Machi, mwaka huu katika shule ya msingi Mkonze” alisema mratibu huyo.

Kwa upande wake mkazi wa kata ya Mkonze Sikuzani Chogo alisema kuwa amefurahishwa na ushiriki wa watumishi wa serikali katika kupanda miti katika shule na kituo cha Afya. “Hata sisi wananchi sasa tunaona umuhimu wa kupanda miti kwenye maeneo yetu” alisema Sikuzani.

Zoezi la upandaji miti katika shule ya msingi Mkonze na kituo cha Afya Mkonze liliratibiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na wadau wengine. Maadhimisho mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kizazi cha usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya sasa na ya baadaye”.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.