• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

WANAWAKE WAPIGA HATUA SEKTA MBALIMBALI

Imewekwa tarehe: December 6th, 2023

Na WMJJWM, Dar es Salaam

Wanawake nchini Tanzania wanaendelea kuwa nguzo imara katika kukuza na kuinua uchumi wa nchi katika sekta mbalimbali; ampapo asilimia thamanini (80%) ya nguvu kazi ya sekta ya kilimo ni wanawake na huzalisha asilimia sitini (60%) ya chakula nchini.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Khamis katika maadhimisho ya siku ya Mama na Mwana Disemba 2, 2023, Jijini Dar es Salaam.

Alisema katika baadhi ya familia, mwanamke ndio mhimili mkuu katika upatikanaji wa chakula, mavazi, malazi, huduma za afya, elimu na maji.

Aidha, Khamis amefafanua kwamba pamoja na majukumu yanayotekelezwa na wanawake katika familia na jamii zetu, bado zipo changamoto zinazowakwamisha ikiwemo vitendo vya ukatili .

“Vitendo vya ukatili vinasababishwa na uwepo wa mila na desturi kandamizi na zenye madhara, uwepo wa mfumo dume, ukosefu wa elimu, ushirikishwaji dhaifu katika ngazi za maamuzi, ukosefu wa elimu ya stadi za maisha pamoja na ukosefu wa mitaji ya utekelezaji wa shughuli za ujasiriamali.” Alisema Mwanaidi.

“Serikali imeendelea kutambua umuhimu wa Wanawake kupewa fursa katika nafasi za Uongozi na kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi mbalimbali za uwakilishi na ufanyaji maamuzi, tunaye  Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa kwanza mwanamke katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini pia yupo  Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Ulimwenguni na takwimu zinaonesha kuwa idadi ya Mawaziri wanawake imeongezeka kutoka asilimia 15 mwaka 2005 hadi asilimia 36 mwaka 2022. Vilevile Wabunge wanawake wameongezeka kutoka asilimia 22 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 37 mwaka 2022.” Alisema Khamisi

Serikali inaendelea kupambana na changamoto ya ukatili katika jamii hususani ukatili dhidi ya wanawake na watoto kupitia afua mbalimbali za kijamii ikiwemo kutungwa kwa sheria za fedha, uanzishwaji wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi na kuendeleza mpango wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.